Ruka hadi kwenye maudhui makuu

NDONDI ZA DUNIA ZAPAMBA MOTO KAZAKHSTAN

Mashindano ya ndondi ya ubingwa wa dunia yanazidi kupamba moto mjini Almaty, Kazakhstan.


Kufikia sasa ni mabondia wawili tu wa Afrika, Efetobor Apochi wa Nigeria uzani wa heavy na Colin Louis wa Mauritius ambao wameshinda mapigano yao na wengine sita kutoka Kenya, Misri, Angola na Nigeria wakashindwa.

Efetobor alimshinda kwa pointi Seyda Keser wa Uturuki naye Louis akamchapa kwa pointi pia Khatuev Salavat wa Norway.

Mabondia sita walioshindwa ni Dan Shisia uzani wa heavy, John Kariuki uzani wa light na Dennis Okoth uzani wa light-welter wote wa Kenya, Vivaldo Rodrigues wa Angola uzani wa fly, Olayinka Yusuff wa Nigeria uzani wa fly na Mohammed Eslam wa Misri uzani wa light-welter aliyeshindwa na Yves Ulysse wa Canada.

Shisia alichapwa na Jim Andreasen wa Denmark kwa pointi, Kariuki akashindwa na Dorjnyambuu Otgondalai wa Mongolia.

Bondia huyo wa Kenya alipata jeraha juu ya jicho lake la kulia hivyo basi refarii akaamua hawezi kuendelea.

Mashabiki wa ndondi mjini Almaty waliachwa vinywa wazi wakishangaa vile bondia wa Uturuki Fatih Keles alivyomshinda Okoth kwa pointi 2-1.

Makocha wa Kenya Albert Matito na George ''Foreman’’ Onyango wanasema mashabiki waliwazomea majaji kwa uamuzi huo wakisema bondia wa Kenya alistahili kushinda kwa sababu alimlemea mwenzake raundi zote.

Vivaldo Rodrigues wa Angola alishindwa kwa pointi na Malik Jackson wa Marekani uzani wa fly, na bondia mwingine wa Nigeria Olayinka Yusuf akashindwa na Charlie Edwards wa England uzani wa fly.

Jumatano wiki hii Raytoin Okwiri wa Kenya na Selemani Kidunda wa Tanzania, wote uzani wa welter, wataingia ulingoni kwa mapigano yao ya kwanza. Okwiri anazipiga na Daniel Lewis wa Australia huku Kidunda akipambana na Mandeep Jangra wa India…

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC