Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MCHEZAJI WA NIGERIA AJERUHIWA VIBAYA..........

Mchezaji soka wa Nigeria, Nosa Igiebor alijeruhiwa vibaya wakati timu yao iliposhambuliwa mjini Addis Ababa baada ya mchuano wao wa mchujo dhidi ya Ethiopia katika kutafuta nafasi ya kushirki kombe la dunia mwaka ujao nchini Brazil.

Mchezaji huyo ambaye huchezea timu ya Real Betis alihitaji matibabu ya dharura mkononi mwake baada ya dirisha la basi walimokuwa kuvunjwa wakati timu hiyo ilipokua inaondoka kutika mji mkuu Addis Ababa.Alijeruhiwa kwa vigae vya glasi.

Nigeria, ilishinda mabao mawili kwa moja na wameripoti tukio hilo kwa Fifa.

"Tunatumai kuwa Fifa itachukua hatua za kinidhamu," alisema makamu rais wa shirikisho la soka la Nigeria Mike Umeh.

"Ni jambo la aibu sana kwa tukio kama hili lilitokea baada ya mechi.”

Ben Alaiya, afisaa wa uhusiano mwema wa timu ya taifa ya Super Eagles alimuunga mkono Umeh katika kulaani tukio hilo.

Alaiya alisema kuwa mashabiki walishambulia basi iliyokuwa imewabeba wachezaji wa timu ya Nigeria kwa mawe ambayo yalivunja mojawapo ya dirisha la basi hivyo kulazimisha wachezaji kukimbilia usalama wao

Waliseama kuwa Igiebor hakubahatika kwani jiwe liligonga mkono wake na kusababisha damu kuvuja sana

Super Eagles wa Nigeria ndio wanaonekana kuwa katika nafasi nzuri ya kufuzu kucheza katika michuano ya kuwania kombe la dunia watakapocheza mechi ya marudiano mjini Calabar tarehe 16 Novemba.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC