Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KUMBE BRANDTS ANARINGIA UBABE WAKE KWA SIMBA.......

NYASI za Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam zinatarajiwa kuwaka moto Jumapili kwa mpambano wa watani wa jadi katika soka ya Tanzania, Simba na Yanga.


Huo utakuwa mchezo wa mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara na leo tunaendelea kukuletea mfululizo wa habari za kuelekea pambano hilo linalobeba picha halisi ya soka ya Tanzania.

Sasa tunamgeukia kocha Mholanzi wa Yanga SC, Ernie Brandts na mechi dhidi ya Simba SC. Endelea.

Beki wa zamani wa kimataifa wa Uholanzi na klabu ya PSV Eindhoven ya Uholanzi, Ernstus ‘Ernie’ Wilhelmus Johannes Brandts, Jumapili ataiongoza Yanga SC kwa mara ya tatu dhidi ya watani wa jadi, Simba SC tangu arithi mikoba ya Mbelgiji Tom Saintfiet Oktoba mwaka jana.

Katika mech mbili za awali, Brandts alipambana na makocha wawili tofauti, kwanza Mserbia Milovan Cirkovick aliyetoa naye sare ya 1-1 na baadaye Mfaransa, Patrick Liewig aliyemfunga mabao 2-0 katika mchezo wa kuhitimisha msimu uliopita, Yanga SC ikikabidhiwa Kombe kwa raha zote- ushindi dhidi ya watani na ubingwa.

Mholanzi huyo aliyetua Yanga SC akitokea APR ya Rwanda aliyoifundisha tangu 2010, Jumapili atapambana na kocha mwingine pia, Alhaj Abdallah Athumani Seif ‘King Kibaden’ ambaye ni mshambuliaji wa zamani wa kimataifa wa Tanzania na Simba SC.

Brandts anajivunia rekodi ya kutofungwa na Yanga SC, lakini hawezi kusahau kipigo cha 1-0 kutoka Kagera Sugar msimu uliopita, ambayo ilikuwa inafundishwa na King Kibaden, aliyeibuka kocha bora wa Ligi Kuu mwishoni mwa msimu.

Brandt alilipa kisasi kwa Kibaden kwa ushindi wa 1-0 pia katika mchezo wa marudiano wa Ligi Kuu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Brandts na Kibaden kila mmoja kamfunga mwenzake mara moja, lakini Mholanzi wa Yanga hajafungwa na Simba SC.

Mtaalamu huyo, alizaliwa Februari 3, mwaka 1956 mjini Nieuw-Dijk, Gelderland, mbali na PSV Eindhoven, alichezea pia Roda JC Kerkrade, MVV Maastricht na De Graafschap.

Brandts aliichezea mechi 28 timu ya taifa ya Uholanzi na kuifungia mabao matano na pia alicheza Fainali za Kombe la Dunia mwaka 1978.
Katika fainali hizo, Raundi ya pili kwenye mechi na Italia, aliweka rekodi ya kuwa mchezaji pekee aliyezifungia mabao timu zote katika mechi moja kwenye fainali za Kombe la Dunia.

Alianza kujifunga dakika ya 18, kisha akaisawazishia Uholanzi dakika ya 50 katika mechi ambayo, mchezaji mwenzake Arie Haan baadaye aliifungia timu yake bao la ushindi na kutoka kifua mbele kwa mabao 2–1.

Alipostaafu soka akawa kocha na katikati ya msimu wa 2007–2008, Brandts aliambiwa hataongezewa mkataba NAC-Breda, licha ya matokeo mazuri ya kushika nafasi ya tatu katika Ligi Kuu Uholanzi (Eredivisie), ingawa uamuzi huo haukuwafurahisha mashabiki wa timu hiyo na nafasi yake akapewa Robert Maaskant kuanzia msimu wa 2008–2009.

Akateuliwa kuwa Kocha wa Rah Ahan mwaka 2009, kabla ya kufukuzwa Desemba 2009 na kuibukia APR ya Rwanda mwaka 2010, ambako alifanya kazi hadi mwaka jana alipohamia Jangwani. Je, Jumapili Brandts ataendelea kuwa kiboko ya Simba SC, au Kibaden atamkumbusha machungu ya Kaitaba mwaka jana? Bila shaka hilo ni jambo la kusubiri na kuona.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC