Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KIPA WA SIMBA APELEKWA JESHINI

KIPA namba moja wa Simba SC, Abbel Dhaira amekwenda kufanyiwa uchunguzi asubuhi hii katika hospitali Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), kitengo cha wanamaji kutokana na matatizo ya msuli wa nyuma ya shingo.

Daktari wa Simba SC, Yassin Gembe amesema leo kwamba Dhaira amekuwa akisumbuliwa na maumivu ya msuli wa nyuma ya shingo tangu kwenye mechi dhidi ya Yanga Jumapili ambayo alifungwa mabao matatu katika sare ya 3-3.
Abbel Dhaira

“Kama utakumbuka katika mechi dhidi ya Yanga alitibiwa tibiwa wakati mchezo unaendelea, ni kutokana na matatizo hayo hayo, kwa hivyo sasa hivi nakwenda naye akafanyiwe uchunguzi,”amesema Gembe asubuhi hii.

Dhaira alitoka dakika ya 35 juzi katika mchezo dhidi ya Coastal Union Uwanja wa Mkwakwani, Tanga baada ya kugongana na mshambuliaji wa Coastal Union, Haruna Moshi ‘Boban’, timu hizo zikitoka sare ya 0-0.


Kipa huyo alisema alipata maumivu madogo kichwani, ambayo anaamini hayatamuweka nje ya uwanja kwa muda mrefu na anataraia kucheza Jumatatu mechi nyingine ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Jumatatu dhidi ya Azam Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Simba SC imerejea Dar es Salaam jana na tayari ipo kambini kwake, Bamba Beach, Kigamboni ikiendelea na maandalizi ya mechi dhidi ya Azam.

Mechi hiyo inatarajiwa kuwa na ushindani mkali kutokana na timu hizo kukabana kileleni, zote zikiwa na pointi 20 sawa na Mbeya City baada ya mechi 10, lakini Simba SC inaizidi Azam wastani mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC