Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KIBADENI AANZA VISINGIZIO, ADAI HAJAPATA FIRST ELEVEN......

Kocha Mkuu wa Simba, Abdallah Kibaden ameweka wazi kuwa bado hajapata kikosi cha kwanza na kudai amebakisha mechi mbili za majaribio ili kupata ‘first eleven’ yake ambapo mechi yao na Yanga Jumapili itakuwa miongoni mwa mechi hizo.


“Simba inahitaji kucheza mechi 10 ambazo zitaniongoza mimi kama kocha kuona nani anastahili kucheza kwenye ‘first eleven’ yangu,” alisema kocha huyo.

Kibaden alisema hivi sasa analazimika kumtumia kila mchezaji kwenye mechi za Ligi Kuu inayoendelea nchini ili kubaini kiwango cha kila mchezaji na kusisitiza kuwa kikosi chake cha kwanza kitajulikana baada ya kucheza michezo 10 ya Ligi Kuu.

Simba itashuka uwanjani Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kucheza dhidi ya Yanga ikiwa ni mchezo wa tisa wa majaribio kwa kocha Kibadeni katika kuangalia uwezo wa wachezaji wake.

“Mechi yetu ya mwisho na Tanzania Prisons (Simba ilishinda 1-0) ndiyo ilikuwa mechi yangu ya nane katika kuwapima vijana wangu, nimebakisha mechi mbili za mwisho ambapo baada ya mechi hizo Simba itakuwa imekamilika kwa kuwa na kikosi cha kwanza,” alisema.

Mechi ya mwisho ya majaribio ya Simba itakuwa dhidi ya Coastal Union ya Tanga ambayo ni mechi ya 10 kwa kikosi hicho huku Kocha Kibaden akidai anahitaji kuwa na kikosi cha kwanza kitakachoitumikia Simba kwa dhati na si vinginevyo.

Hata hivyo hii siyo mara ya kwanza kwa kocha Kibaden kutoa kauli hiyo ya kutafuta kikosi chake cha kwanza kwani amekuwa akizungumza mara kwa mara kwamba baada ya kucheza mechi kumi za Ligi Kuu siyo mechi za kirafiki ndiyo atakuwa amepata kikosi chake cha kwanza kwani atakuwa amepata nafasi kubwa ya kuwasoma wachezaji wake wote, ambapo karibu kila mechi amekuwa akiwapa nafasi wachezaji tofauti.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC