Ruka hadi kwenye maudhui makuu

HOFU YA KIPIGO DHIDI YA YANGA J,PILI, SIMBA WALIKIMBIA JIJI.......

Wakati  mabingwa wa ligi kuu ya Bara, Yanga jana walitua kisiwani Pemba kwa ajili ya maandalizi ya mechi yao dhidi ya Simba itakayopigwa kwenye Uwanja wa Taifa Jumapili, Wekundu wa Msimbazi wakihamisha kambi kutoka Bamba Beach na kwenda Bagamoyo.


Simba walilala 2-0 katika mechi yao iliyopita ya ligi lakini hivi sasa wakiwa na kinara wa kufumania nyavu, Mrundi Amisi Tambwe, hawako tayari kufungwa na kukabidhi uongozi wa ligi kwa Yanga.

Akizungumza jana kwa njia ya simu kocha msaidizi wa Yanga, Fred Minziro alisema kikosi chake kiliwasili Pemba jana kwa ajili ya kambi hiyo.

Alisema timu hiyo imeamua kupiga kambi visiwani humo ili kukwepa usumbufu, ikiwa ni pamoja na kutaka kuwapa wachezaji nafasi ya kufanya mazoezi kwa uhuru zaidi tofauti wanapokuwa Dar es Salaam.

Alisema timu iliingia Dar juzi ikitokea Kagera ilikoshinda 2-1 dhidi ya Kagera Sugar na jana asubuhi wakawasili Pemba ambako sasa akili yao iko kwenye pambano hilo la watani wa jadi.

"Timu iko vizuri, wachezaji wote wanaendelea vizuri na mazoezi kwa ajili ya kujiandaa na mechi hiyo," alisema na kuongeza kuwa wanatarajia kuwashangaza Simba.
Alisema wachezaji wote sasa wako poa baada ya majeruhi wa muda mrefu Salum Telela naye kurejea mazoezini.

Minziro alisema watakuwa Pemba kwa takribani siku nne kabla ya kurejea Dar kwa ajili ya mechi hiyo.

Hata hivyo, kwa mujibu wa habari za ndani, timu hiyo inapanga kurejea jijini Dar kwa ndege asubuhi ya siku ya mechi hiyo.

Kocha msaidizi wa Simba, Jamhuri Kihwelu 'Julio' alisema jana kuwa Simba ambayo imekuwa kambini Bamba Beach, Kigamboni imehama mahala hapo na kwenda Bagamoyo jana jioni. Julio alisema Yanga watakiona cha moto katika mechi hiyo kwenye Uwanja wa Taifa.

Simba inaendelea kuongoza ligi hiyo kwa pointi 18 ikifuatiwa na Azam na Mbeya City zenye pointi 17 kila moja. Yanga ni ya nne ikiwa na pointi 15. Hata hivyo, Simba na Yanga zimecheza mechi moja pungufu katika ligi hiyo ambayo imeingia katika raundi ya tisa.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC