Ruka hadi kwenye maudhui makuu

HAMISI KIIZA AMGWAYA TAMBWE, UFUNGAJI BORA

Mshambuliaji  Mganda Hamis Kiiza wa Yanga amesema kuwa kwa sasa hawazii kiatu cha dhahabu cha mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu huu, bali mawazo yake yamejikita katika kuhakikisha anaisaidia timu yake kutetea ubingwa wa ligi hiyo.

Kiiza alisema baada ya mazoezi ya Yanga kwenye uwanja wa Shule ya Sekondari Loyola uliopo Mabibo jijini Dar es Salaam jana kuwa hashindani na wachezaji wengine kusaka zawadi ya mfungaji bora bali anasaka mafanikio ya kikosi cha 'Wanajangwani'.


"Kikubwa ni kutetea ubingwa, zawadi ya mfungaji bora siifikirii sana kwa sasa. Naamini kufunga magoli mengi kutaisaidia timu yetu kuibuka bingwa tena. Na tukishakuwa na magoli mengi, kiatu cha dhababu kitakuja chenyewe, alisema Kiiza ambaye juzi alifunga goli moja na kufikisha magoli nane katika michezo saba ya ligi hiyo msimu huu.
Amemfikia aliyekuwa kinara pekee, Amisi Tambwe wa Simba.

Katika hatua nyingine, kiungo 'fundi' Haruna Niyonzima 'Fabregas' , aliyeukosa mchezo wa juzi walioshinda 3-0 dhidi ya Mgambo JKT kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kutokana na matatizo ya kifamilia, anatarajiwa kurejea mazoezini leo.

Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Yanga, Baraka Kizuguto, kiungo huyo atarejea dimbani leo kujiandaa kwa mchezo wao wa kesho dhidi ya JKT Ruvu ya Pwani utakaopigwa kwenye Uwanja wa Taifa baada ya kumalizika kwa siku tatu za ruhusa aliyoomba kwa ajili ya kumaliza matatizo ya kifamilia yaliyokuwa yanamkabili.

Niyonzima alirejea kwao Rwanda siku nne zilizopita na alitarajiwa kurudi jana kuungana na kikosi cha kocha Mholanzi Ernie Brandts.

Wachezaji wengine wa Yanga ambao walikosa mazoezi ya jana yaliyofanyika kwa saa mbili kuanzia saa 3:00 asubuhi kutokana na majeraha ni pamoja na kiungo Nizar Khalfan, beki wa pembeni Juma Abdul na kiungo Salum Telela.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC