Ruka hadi kwenye maudhui makuu

HAIJAPATA KUTOKEA BARANI AFRIKA...............

Furaha ya kupita kiasi ndiyo iliyosababisha zaidi ya watu 20 kuzimia uwanjani wakati walipokuwa wakishuhudia mchezo wa Ligi Kuu kati ya Simba na Yanga uliofanyika juzi Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Katika mchezo huo uliokuwa umejaa na presha kubwa kuanzia kwa wachezaji hadi kwa mashabiki wa pande zote mbili ulimalizika kwa timu hizo kufungana mabao 3-3.


Kwa mujibu wa Kiongozi wa Kikosi cha Maafa cha Msalaba Mwekundu, Bushiri Mgamba aliyekuwa akiongoza kikosi cha huduma ya kwanza uwanjani hapo alisema kuwa sababu kubwa ya watu hao kuzimia ilitokana na kuwa na furaha kupita kiasi.

Alisema baadhi ya watu wanapokuwa na furaha kupita kiasi wanapatwa na hali hiyo, lakini siyo kwa kila mtu na ndiyo maana hiyo juzi waliozimia uwanjani hapo walikuwa wachache ingawa waliokuwa na furaha walikuwa ni wengi.

“Hali hiyo pia inaweza kuzuilika, ambapo ni mtu mwenyewe anaweza kujizuia ili isimpate,” alisema Mgamba.

Hata hivyo, mmoja wa viongozi wa kikosi hicho cha maafa cha Msalaba Mwekundu ambaye pia aliwahi kuwa daktari wa timu ya Yanga, Juma Sufiani aliliambia gazeti hili kuwa katika mechi hiyo watu wengi walizimia kipindi cha kwanza.

Alisema watu hao walipatwa na hali hiyo baada ya Yanga kufunga bao la pili na lile la tatu, mabao ambayo yalipachikwa wavuni na Hamis Kiiza.

“Mabao hayo yalisababisha watu hao kuzimia ambao wengi wao walikuwa ni mashabiki wa Yanga kwani walikuwa na furaha kupita kiasi na kujikuta wakizimia.

“Pia katika kipindi cha pili cha mchezo huo hali hiyo ilihamia upande wa mashabiki wa Simba, ambapo napo baadhi yao walizimia, ilikuwa ni baada ya timu hiyo kupata bao la pili na la tatu yaliyofungwa na Joseph Owino na Gilbert Kaze,” alisema Sufiani.

Aliongeza kuwa, ‘‘Watu hao walipatiwa huduma uwanjani hapo na hali zao ziliendelea vizuri na hadi kufikia jana kulikuwa hakuna taarifa yoyote mbaya.”

Naye Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Angetile Osiah aliliambia gazeti hili kuwa hali hiyo ilikuwa ni ya kushangaza, lakini walikuwa wamejipanga vilivyo kukabiliana na tukio lolote ambalo lingetokea uwanjani hapo.

“Tulikuwa tumejipanga vizuri kabisa, watu wa huduma ya kwanza walikuwapo wa kutosha na wote waliopatwa na hali hiyo walipatiwa huduma, ni matumaini yetu kuwa hali zao ni nzuri kwani hadi sasa hatuna taarifa yoyote mbaya,” alisema Osiah.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...