Ruka hadi kwenye maudhui makuu

FERGUSON AMUUMBUA BECKHAM

Aliyekuwa meneja wa klabu ya Manchester United ya Uingereza Sir Alex Ferguson amesema David Beckham alilazimika kuondoka katika klabu hiyo kutokana na tabia yake ya kujiona ni mkubwa kuliko meneja wake.

Katika kitabu kipya kuhusu historia ya maisha yake Ferguson amesema enzi za uongozi wake walitofautiana na Beckham kutokana na kumkosoa kuhusiana na kiwango chake katika matokeo ya ligi ya FA 2003.


Mchezaji huyo alionekana kuwa na msimamo unaoonyesha kujiona mkubwa na kutokubali maelekezo .

Furguson amesema kuwa tabia ya Beckham ilionekana kubadilika tangia alipomuoa mwanamuziki maarufu wa miondoko ya pop Victoria kutoka kundi la Spice Girls

"David ni mchezaji pekee ambaye nilimuwezesha kumuweka katika mazingira ya umaarufu wa soka kidunia, lakini sikufurahishwa na maisha ya umaarufu wake na hasa kujiona yeye ni bora zaidi' alisema Ferguson.

Ferguson amesema haijalishi ni Alex Furguson ama Pete the plumber, lakini mamlaka ni mamlaka tu, hangeweza kuwa na mchezaji ambaye haheshimu mamlaka,nadhan kama ni kuondoka ni bora alivyoondoka tu.

Beckham aliyeshinda mara sita katika ligi ya Premier ya uingereza,vikombe viwili vya FA na moja katika Champions League akiwa na klabu hiyo baadaye aliuzwa kwa Real Madrid kwa dola million 25 katika msimu wa joto 2003,kabla ya kwenda nchini Marekani kuchezea klabu ya LA Galaxy.

Sir Alex Ferguson yeye amestaafu mwezi May mwaka huu umeneja katika klabu hiyo ya Manchester huku akiwa ni miongoni mwa mameneja walifikia mafanikio makubwa katika historia ya kuiongoza timu hiyo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC