Ruka hadi kwenye maudhui makuu

BRANDTS NAYE KUTUPIWA VIRAGO YANGA.

UONGOZI wa Yanga SC unafuatilia mwenendo wa timu kwa ujumla na utendaji wa kocha wake, Mholanzi Ernstus ‘Ernie’ Wilhelmus Johannes Brandts kwa mechi zilizobaki za mzunguko wa kwanza na baada ya hapo itaamua kumuongeza Mkataba au kuachana naye mwalimu huyo.
Brandts ametimiza mwaka mmoja wa Mkataba wake Yanga mwezi huu, lakini kuhusu Mkataba mpya ametakiwa kusubiri hadi mwisho wa mzunguko wa kwanza wa ligi mwezi ujao.

Yanga SC hawajaonyesha wasiwasi juu ya uwezo wa Brandts katika kufundisha, lakini wanatilia shaka mambo matatu; sera zake, usimamiaji wake wa nidhamu ya wachezaji na kutokuwa na maamuzi ya haraka.

Brandts analaumiwa kwa kitendo cha kuruhusu wachezaji wasikae kambini muda mrefu, akidai wachezaji si wafungwa wanatakiwa huru na mara nyingi Yanga imekuwa ikiingia kambini siku mbili kabla ya mechi.

Kwa kuzingatia wapinzani wao wa jadi, Simba SC wako kambini muda wote Bamba Beach, Kigamboni, Dar es Salaam, Yanga nao wanaona hata kwao inawezekana, lakini Brandts amekuwa akikataa utaratibu huo.


Yanga SC pia wana wasiwasi Brandts ameshindwa kusimamia vyema nidhamu ya wachezaji katika timu hiyo, jambo ambalo limesababisha baadhi yao viwango kushuka.

Aidha, Brandts analaumiwa kutokuwa na maamuzi ya haraka hususan katika kubadilisha timu na wachezaji, mara anapoona aliowapa majukumu wanashindwa kuyatekeleza ipasavyo na mambo hayo matatu ndiyo yanabeba mustakabali wake katika timu hiyo hivi sasa.

“Aliona kabisa Barthez (Ally Mustafa) amemtumia muda mrefu, kachoka, lakini akashindwa kumpumzisha hadi akaja kuigharimu timu. Hata upangaji wake wa timu, namna anavyofanya subs (mabadiliko) ni mashaka matupu,”kilisema chanzo kutoka Yanga jana.

Brandts alibadilisha karibu nusu ya kikosi chake cha kwanza baada ya sare ya 3-3 na Simba SC Oktoba 20, timu ikitoka kuongoza 3-0 hadi mapumziko na tangu hapo, Yanga imeshinda mabao matatu mechi mbili mfululizo bila kuruhusu nyavu zake kuguswa, langoni akisimama Deo Munishi ‘Dida’.

Tayari Yanga SC imeachwa hatua katika kadhaa katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu msimu huu, wakiwa wanazidiwa pointi moja na Azam FC na Mbeya City wanaokabana kileleni kwa pointi zao 23 kila timu. Azam ipo kileleni kwa wastani wake mzuri wa mabao.

Yanga inatarajiwa kushuka tena dimbani kesho kumenyana na JKT Ruvu, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, wakati leo wapinzani wao, Simba SC wanamenyana na Kagera Sugar kwenye Uwanja huo.

Brandts, beki wa zamani wa kimataifa wa Uholanzi na klabu ya PSV Eindhoven ya Uholanzi, alirithi mikoba ya Mbelgiji Tom Saintfiet Oktoba mwaka jana, akitokea APR ya Rwanda aliyoifundisha tangu 2010.
Mtaalamu huyo, aliyezaliwa Februari 3, mwaka 1956 mjini Nieuw-Dijk, Gelderland, mbali na PSV Eindhoven, awali alichezea klabu za Roda JC Kerkrade, MVV Maastricht na De Graafschap za kwao.

Brandts aliichezea mechi 28 timu ya taifa ya Uholanzi na kuifungia mabao matano na pia alicheza Fainali za Kombe la Dunia mwaka 1978.
Katika fainali hizo, Raundi ya pili kwenye mechi na Italia, aliweka rekodi ya kuwa mchezaji pekee aliyezifungia mabao timu zote katika mechi moja kwenye fainali za Kombe la Dunia.

Alianza kujifunga dakika ya 18, kisha akaisawazishia Uholanzi dakika ya 50 katika mechi ambayo, mchezaji mwenzake Arie Haan baadaye aliifungia timu yake bao la ushindi na kutoka kifua mbele kwa mabao 2–1.

Alipostaafu soka akawa kocha na katikati ya msimu wa 2007–2008, Brandts aliambiwa hataongezewa mkataba NAC-Breda, licha ya matokeo mazuri ya kushika nafasi ya tatu katika Ligi Kuu Uholanzi (Eredivisie), ingawa uamuzi huo haukuwafurahisha mashabiki wa timu hiyo na nafasi yake akapewa Robert Maaskant kuanzia msimu wa 2008–2009.

Akateuliwa kuwa Kocha wa Rah Ahan mwaka 2009, kabla ya kufukuzwa Desemba 2009 na kuibukia APR ya Rwanda mwaka 2010, ambako alifanya kazi hadi mwaka jana alipohamia Jangwani.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC