Ruka hadi kwenye maudhui makuu

BARTHEZ AREJESHWA YANGA........

Benchi la ufundi la Yanga limemsafisha kipa wake namba moja, Ally Mustapha ‘Barthez’ dhidi ya shutuma anazotupiwa na mashabiki wa timu hiyo tangu siku ya Jumapili baada ya kumalizika kwa mechi ya Ligi Kuu dhidi ya Simba.

Mashabiki hao wanamshutumu Barthez kuwa alichangia timu hiyo ishindwe kuibuka na ushindi katika mchezo huo uliomalizika kwa sare ya bao 3-3 ikiwa ni baada ya Yanga iliyokuwa ikiongoza kwa mabao 3-0 katika kipindi cha kwanza kuruhusu wapinzani wao hao wa jadi Simba kusawazisha mabao yote kipindi cha pili cha mchezo huo.


Hali hiyo iliwafanya mashabiki hao kuanza kumshutumu Barthez kuwa ndiye aliyeihujumu timu yao katika mchezo huo ambao ulikuwa na ushindani mkubwa.

Kocha msaidizi wa Yanga, Felix Minziro amesema kuwa wanaomshutumu kipa huyo hawajui mpira kwani hali iliyotokea katika mechi hiyo ni ya kimchezo ambayo inaweza kutokea kwa timu yoyote ile.

Alisema shutuma hizo anazotupiwa Barthez na baadhi ya mashabiki wa timu hizo hazina ukweli wowote isipokuwa zimelenga kumchafua, lakini wao kama benchi la ufundi la timu hiyo bado wana imani naye na wataendelea kumwamini kama walivyokuwa wakimwamini hapo awali.

“Matokeo kama hayo siyo ya kwanza kutokea kwa Yanga, timu inaweza kuongoza kwa muda mwingi, lakini dakika chache tu kabla ya kumalizika kwa mchezo matokeo yakabadilika.

“Hivyo mashabiki wetu wanapaswa kulijua hilo na tunawaomba waendelee kumuunga mkono Barthez, pia wanatakiwa kutambua kuwa  maotokeo ya Jumapili dhidi ya Simba ni ya kawaida katika soka,” alisema Minziro.

Aliongeza kuwa,”Kutoonekana kwa Barthez katika mechi yetu dhidi ya Rhino Rangers jana (juzi) ni maamuzi ya benchi la ufundi,” alisema Minziro.

Katika hatua nyingine Minziro aliongeza kuwa timu hiyo itaendelea na mazoezi yake leo kwa ajili ya kujiandaa na mechi zake za Ligi Kuu zilizobakia

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC