Ruka hadi kwenye maudhui makuu

AL AHLY USO KWA USO NA ORLANDO PIRATES

Al ahly wanajiandaa kumenyana na Orlando Pirates
Klabu ya soka ya Misri, Al-Ahly iko kifua mbele katika kutetea ubingwa wao wa ligi ya klabu bingwa Afrika baada ya kuicharaza klabu ya Cameroon ya Coton Sport katika penalty ili kuweza kufika fainali.
Klabu hiyo ya Cairo ilishinda kwa ujumla wa mabao sita saba kwenye mechi iliyochezwa katika eneo la El-Gouna baada ya mechi ukamilia kwa sare ya bao maoja kwa moja.
Matokeo sawa na hayo yalishuhudiwa kwenye mechi ya mkondo wa kwanza, iliyomalizika kwa mabao mawili kwa mawili.

Ahly itakutana na Orlando Pirates wa Afrika Kusini katika fainali itakayokuwa na mikondo miwili mwezi ujao.
Abdullah Al Saied aliingiza bao baada ya dakika tatu ya kuanza kwa mchezo na kuipa Misri mwanzo mzuri wa mechi , na kisha kuingiza bao lengine.
Ahly, ambayo haikushiriki mechi tatu za kimataifa, iliyohusisha mechi ya Misri ambayo ilishindwa vibaya sana na Ghana, ilipata nafasi nzuri za kuendeleza ushindi wao wakati wa kipindi cha kwanza cha mchuano.
Mchezaji Alexis Yougouda alifanikiwa kuingiza bao lake la saba
Wakati wa mchuano huo, Mohamed Aboutrika alikosa bao lake la kwanza lakini wachezaji wenzake walifanikiwa kuingiza mabao baadaye.
Mechi hiyo ilichezwa bila ya mashabiki baada ya kupigwa marufuku kushuhudia mechi za klabu yao, kutokana na ghasia za hivi karibuni.
Kocha wao Mohamed Youssef pia alilazimika kujionea mechi akiwa nje ya uwanja baada ya kuondolewa uwanjani wakati wa mkondo wa kwanza wa mecih hizo mjini Garoua wiki mbili zilizopita.
Ahly wameshinda ubingwa wa ligi hiyo mara saba awali, na kuifanya kuwa klabu yenye kufanikiwa zaidi barani Afrika.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...