JKT Tanzania yashindwa kuishusha Yanga kileleni
Timu ya JKT Tanzania imeshindwa kuishusha Yanga SC kileleni baada ya kufungwa bao 1-0 na Dodoma Jiji uwanja wa Meja Isamuyo Mbweni jijini Dar es Salaam mchezo wa Ligi Kuu bara.
Bao pekee la Dodoma Jiji limefungwa na mshambuliaji wake hatari Wiliam Edgar dakika ya 50, kwa matokeo hayo JKT Tanzania inaendelea kubaki nafasi ya pili na pointi zao 21 wakati Yanga ikiongoza na alama 22.
