Kennedy Musonda apata timu Israel
MSHAMBULIAJI wa Kimataifa wa Zambia, Kennedy Musonda amejiunga na klabu ya Hapoel Ramat Gan Givatayim F.C ya Israel baada ya kuachana na Yanga ya Tanzania.
Taarifa ya Hapoel RGG F.C imesema kwamba Musonda atawasili wakati wowote kwa ajili ya vipimo vya afya kabla ya kutambulishwa rasmi.
Kwa sasa Hapoel Ramat Gan Givatayim F.C inayofahamika kwa jina la utani la ‘The Jordanians’ inashiriki Liga Leumit, ligi ya pili kwa ukubwa baada ya Ligi Kuu ya Israel.
Musonda alipost jana kwenye ukurasa wake kuaga Yanga SC baada ya misimu miwili na nusu ya kuitumikia klabu hiyo ya Jangwani.

