Opah Clement amfuata Singano Mexico
Mtanzania,Opah Clement Tukumbuke Sanga amejiunga na klabu FC Juarez ya Mexico baada ya kuachana na Henin FC ya China.
Opah atakuwa pamoja na Mtanzania mwingine Julitha Singano ambaye pia anaitumikia klabu hiyo.
Nyota huyo aliwahi kuitumikia Simba Queens na Besiktas ya Uturuki.
