Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Bubah Jammeh atambulishwa Yanga

Machapisho ya hivi karibuni

Simba yamalizana na straika la Ivory Coast

Simba amekamilisha usajili wa mshambuliaji raia wa Ivory Coast, Mofossé Trésor Karidioula, katika dirisha dogo la usajili kwa ajili ya msimu huu wa Ligi Kuu Tanzania Bara Na Mashindano Ya kimataifa. Karidioula, mwenye umri wa miaka 27, amejiunga na kikosi cha simba huku akiwa na rekodi ya kucheza katika ligi mbalimbali za Afrika na uzoefu wa kimataifa. Mchezaji huyo aliitumikia klabu ya Haras El Hodood ya Misri msimu uliopita kabla ya kuwa huru, na sasa anaendelea na safari yake mpya akiwa Simba. Kabla ya kuichezea Misri, Karidioula alionyesha ubora wake akicheza kwa vilabu kama Williamsville AC na ASEC Mimosas ya Ivory Coast, Simba wamemsajili akitokea Marumo Gallants FC ya Afrika Kusini. Karidioula anacheza katika nafasi za mbele kama winger au mshambuliaji, akijulikana kwa kasi yake, mbinu bora ya kuvunja safu za ulinzi na uwezo wa kufunga na kusaidia mabao. Uzoefu wake mkubwa uwanjani unatarajiwa kuongeza nguvu kubwa katika safu ya ushambuliaji ya Simba, huku akiwa amevaa jezi namb...

Al Ahly wafanya mazoezi ya kuimaliza Yanga kesho

Al Ahly katika mazoezi yao ya mwisho leo kuelekea mchezo wao wa Marudiano dhidi ya Yanga hapo Kesho. Yanga itacheza kesho saa 10 jioni Katika uwanja wa New Aaman Complex Zanzibar.

JKT Tanzania yashindwa kuishusha Yanga kileleni

Timu ya JKT Tanzania imeshindwa kuishusha Yanga SC kileleni baada ya kufungwa bao 1-0 na Dodoma Jiji uwanja wa Meja Isamuyo Mbweni jijini Dar es Salaam mchezo wa Ligi Kuu bara. Bao pekee la Dodoma Jiji limefungwa na mshambuliaji wake hatari Wiliam Edgar dakika ya 50, kwa matokeo hayo JKT Tanzania inaendelea kubaki nafasi ya pili na pointi zao 21 wakati Yanga ikiongoza na alama 22. Wiliam Edgar

Yanga Princess yazidi kuipumulia Simba Queens kileleni

Yanga Princess imeendelea kuifukuzia Simba Queens katika msimamo wa Ligi Kuu ya wanawake Tanzania bara, baada ya leo kuifunga Bunda Queens mabao 3-1 uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza. Magoli ya Yanga Princess yamefungwa na Jeannine Mukandayisenga aliyefunga mabao mawili na Aisha Djafar wakati bao la Bunda Queens limefungwa na Kulwa Rocket. Yanga Princess anamaliza raundi ya kwanza na ushindi mnono ugenini huku akiendelea kuwa nafasi ya pili chini ya Simba Queens. Bunda Queens wameganda pale pale wanaruhusu vipigo nyumbani mfululizo.

Clara Luvanga apiga hat trick nyingine Al Nassr

Mshambuliaji wa Kimataifa wa Tanzania Clara Luvanga hii leo ameifungia Hat Trick Klabu yake ya Al Nassr Women na kuisaidia kushinda 7-1 dhidi ya Eastern Flames kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Wanawake nchini Saudi Arabia . . Clara Luvanga amefikisha mabao 15 kwenye Ligi hiyo akiwa ndiye kinara wa mabao huku Klabu yake ikishika nafasi ya kwanza kwenye Msimamo wa Ligi ikiwa na pointi 24 baada ya kucheza michezo minane.

Okwi aipongeza Yanga kumsajili Okello

Mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Uganda, Emmanuel Anorld Okwi, amefunguka na kuipongeza klabu ya Yanga kuinasa saini ya kiungo wa ushambuliaji, Allan Okello huku akidai kuwa wamefanya kazi kubwa na wamepata mchezaji bora. Kwani sio kitu rahisi kumshawishi rais wa klabu ya Vipers, Lawrence Mulindwa ambaye alikuwa akiamini watamuuza Okello barani Ulaya au nchi za Afrika ya Kaskazini kutokana na uwezo alionao. "Kwenye ukweli lazima useme kuwa va uongozi wa Yanga unastahili pongezi kwa usajii wa nyota Allan Okelo wa Uganda. Huku ni kukomaa kwa viongozi wa Yanga, kingine ni kitendo cha Rais wa Yanga, Eng. Hersi Saidi kuingilia kati mwenyewe kimemfanya Mulindwa kuwa mpole''. Alisema Okwi, ambaye pia amewahi kukipiga Yanga SC.