Simba amekamilisha usajili wa mshambuliaji raia wa Ivory Coast, Mofossé Trésor Karidioula, katika dirisha dogo la usajili kwa ajili ya msimu huu wa Ligi Kuu Tanzania Bara Na Mashindano Ya kimataifa. Karidioula, mwenye umri wa miaka 27, amejiunga na kikosi cha simba huku akiwa na rekodi ya kucheza katika ligi mbalimbali za Afrika na uzoefu wa kimataifa. Mchezaji huyo aliitumikia klabu ya Haras El Hodood ya Misri msimu uliopita kabla ya kuwa huru, na sasa anaendelea na safari yake mpya akiwa Simba. Kabla ya kuichezea Misri, Karidioula alionyesha ubora wake akicheza kwa vilabu kama Williamsville AC na ASEC Mimosas ya Ivory Coast, Simba wamemsajili akitokea Marumo Gallants FC ya Afrika Kusini. Karidioula anacheza katika nafasi za mbele kama winger au mshambuliaji, akijulikana kwa kasi yake, mbinu bora ya kuvunja safu za ulinzi na uwezo wa kufunga na kusaidia mabao. Uzoefu wake mkubwa uwanjani unatarajiwa kuongeza nguvu kubwa katika safu ya ushambuliaji ya Simba, huku akiwa amevaa jezi namb...
MAMBO UWANJANI
Kwa habari na matangazo tunapatikana Kariakoo jijini Dar es Salaam au piga +255 652 626627 au +255 755 522 216 barua pepe princehoza@gmail.com