Inaandikwa na Fikiri Salum
MUSA aliishi miaka ya 1250 hivi KK akawa kiongozi wa wana Israel walipoondoka nchini Misri kukimbilia nchi ya Kanaani iliyoitwa Palestina na Israel baadaye.
Hasa Torati na vitabu vingine vya biblia vinasimulia habari zake, pia Kurani inamtaja Musa katika Aya 502, Waisrael waliishi Misri kama wageni tu zaidi ya miaka mia nne (Mdo 7-6-16 wakiongezeka kiasi cha kuwatisha wenyeji wao ambao walianza kuwafanya watumwa mwaka 1,300 hivi KK, kwa mujibu wa biblia, katika kuwakomboa utumwani, Mungu alijionesha mtetezi wa haki za masikini.
Pamoja na kushurutishwa kufanya kazi walizozipenda, ilitolewa amri ya kuua watoto wote wa kiume, ingawa mpango huo haukutekelezwa sawa sawa (KUT 1:7-22).
Mmoja kati ya watoto waliookolewa katika mpango wa kuua watoto wa kiume ni Musa wa kabila la Lawi (KUT 2:1-10; EB 11:23: Mdo 7:17-22), mama wa Musa alimficha mtoto halafu akamweka ndani ya kikapu mtoni.
Hatimaye mtoto akaokotwa na binti Farao na kulelewa kama mtoto wa Kifalme, lakini alijua asili yake, baadaye akawa Afisa wa Kimisri alipaswa kukimbilia Jangwani kwa kabila la Wamidiami akaolea huko (KUT 2:11-22: EB 11:24-27: Mdo 7:23-29). alipokuwa kwenye mlima Sinai akaitwa na Mungu kutoka ndani ya kichaka kinachowaka moto bila kuteketea.
Mungu alimchagua kurudi Misri na kuongoza watu wake katika utumwa wa Farao, Mungu akasisitiza aende mwenyewe, naye atatumia uwezo wake wa Kimungu kumlazimisha Farao.
Kadiri Musa alivyoomba, Mungu alimfunulia jina lake takatifu YHWH ambalo linaeleweka kiasi tu, kama vile fumbo la Mungu mwenyewe (KUT 2:23-20: Mdo 7;30-35.
MAPIGO YA WAMISRI
Mungu alipomtuma Musa kwa Farao alijua tayari huyo atakataa kuwaruhusu Waisrael waende zao, mpaka aone mapigo yake kwa Wamisri, kwa kuwa ulihitajika muda kuleta ukombozi iliwabidi Waisrael wawe na imani na subira hadi ahadi za Mungu zitimie.
Waisrael walianza kunung' unika (KUT 5:1-6:1) hata hivyo Mungu akaendelea na mpango wake, maajabu aliyoyatenda huwa yanatokea Misri lakini si yote kwa wakati mmoja wala si kwa kiasi kile alichosababidha Musa kwa fimbo yake (KUT 6:28-7:7).
Tuna orodha hayo lakini kwa kawaida yanahesabiwa kumi maji ya mto Naili kuwa mekundu kama damu, vyura kujaa nchi, chawa, nzi, tauni, majipu, mvua ya mawe, nzige, Giza na hatimaye kifo cha wazaliwa wa kwanza wa kiume wa watu na wanyama.
Adhabu hizo ziliwapata Wamisri, lakini si Waisrael hivyo ilikuwa wazi kuwa Mungu anagua watu wake na watu waovu, katika pigo la kumi Waisrael waliopolewa kwa kuipaka milango yao damu ya mwanakondoo (KUT 11;1+10 Mdo 7:36-37: EB 11:28).
Hivyo Mungu aliwaandaa watu kupokea imani kwa Yesu Kristo, mwanakondoo wa kweli na mkombozi wa waliokuwa watumwa wa dhambi, shetani na kifo (Yoh 19:36: /Kar 5:7;/ Pet 1:18-20) hiyo ni wazi katika ibada iliyoagizwa ifanyike kila mwaka (KUT 12:1-14) yaani Waisrael wale nyuma ya mwanakondoo dume asiye na hila, pamoja na mkate usiotiwa chachu na mboga ya majani machungu.
Yesu akaifanya ibada hiyo iwe ibada kwa Agano jipya la milele, akiagiza tuifanye kwa ukumbusho wake, si tena kwa ukumbusho wa kutoka Misri (1 Kor 11:28-26).
SAFARI YA KWENDA NCHI YA AHADI
KUT 12:24-42 inasimulia Waisrael wote walivyokimbia Misri pamoja na mifugo yao waliposikia mayowe kutoka nyumba za majirani wao wote.
INAENDELEA
