Inaandikwa na Fikiri Salum
DOMENI+ Eukaryota, Himaya- Animalis (wanyama) Fails: chordata (wanyama) au (wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni) Ngeli; Mamalia (wanyama wenye viwele wanaonyonyesha wadogo wao) Oda: primatei (wanyama wanaofanana kiasi na binadamu).
Familia ya Hominoidea au (wanyama kama binadamu) Fakilia: hominidea (wako na mnasaba na binadamu).
Nusufamilia: hominidea (wanaofanana sana na binadamu) Jenasi; Homo, Linnaeus, 1758 Spishi! H Sapiens, Linnaeus 1758 Numspishi: H S, Sapiens.
Binadamu (pia mwanadamu) ni neno linalomaanisha mwana wa Adamu anayeaminiwa na dini ya Uyahudi, Ukristo na Uislamu kuwa ndiye mtu wa kwanza.
BINADAMU KADIRI YA SAYANSI
Kisayansi jina hilo linaweza kutumika kwa maana ya Homo Sapiens Ili kumtofautisha na viumbe wengine wa Jenasi Homo ambao wote walitoweka walau miaka 12,000 hivi iliyopita.
Watu wote walioko leo hii ni spishi Ile Ile na tofauti zinazoonekana kati ya maumbile yao katika sehemu mbalimbali za dunia ni kidogo tu.
Utafiti juu ya DNA umethibitisha kwamba binadamu wote wametokana na watu waliokiwepo Afrika walau miaka 250,000 hivi iliyopita.
Kwa namna ya pekee, upimaji wa DNA ya mviringo, ambayo kila mmoja anarithi kwa mama tu, ulionyesha kuwa binadamu wote waliopo duniani wanachangia mama mmoja aliyewahi kuishi miaka 130,000 hivi iliyopita.
Halafu upimaji wa kromosomu Y, ambayo kila mwanamume anarithi kwa baba tu, ulionyesha kuwa wanaume wote wanachangia baba mmoja aliyewahi kuishi walau miaka 70,000 hivi iliyopita, kidogo kabla ya baadhi ya watu kuanza kuhama bara la Afrika na kuenea Asia labda kufuata pwani za bahari ya Hindi.
Hata hivyo, miaka hii ya mwisho imegundulika katika baadhi ya wanaume wenye asili ya makabila ya Wabangwa na Wambo (Cameroon), Afrika ya Kati) aina ya Kromosomu Y, tofauti sana na Ile ya wanaume wengine wote waliowahi kupimwa, kiasi kwamba kukadiria imetofautiana miaka 350,000 hivi iliyopita.
Vilevile upimaji wa DNA ya mstari kwa jumla umeonyesha uwezekano wa kwamba baadhi ya binadamu wa leo, wale wasio wa kusini mwa Sahara, wana asilimia 1-6 ya urithi wa kibiolojia kutoka kwa aina nyingine za Homo, hususani Homoneanserthlensis, Ile ya pango la Denisova na Ile iliyorithiwa na baadhi ya watu wa visiwa vya Andaman (India).
Kama hao waliweza kweli kuzaliana na Homo Sapiens maana yake walikuwa spishi moja na yeye, hapo asili ya binadamu inatakiwa kuhesabiwa ya zamani zaidi sana kuliko 200,000 iliyofikiriwa kwanza.
INAENDELEA
