Penzi la Wastara(43) na Dudubaya(51) limeanza kuchukua sura mpya baada ya Wastara kutoa kauli inayodokeza tayari amepanga kufunga ndoa na Dudubaya ambaye ni mwanamuziki mkongwe wa kizazi kipya(Bongofleva). Wastara ndie alianza kuweka wazi penzi lao kisha Dudubaya kuthibitisha baadaye
Wastara ambaye baba yake alikuwa mwarabu, hata hivyo haijajulikana bado ndoa ya safari hii wamepanga iwe ya dini gani kwani yeye Wastara ni muislamu wakati Dudubaya ambaye jina lake halisi ni Godfrey Tumaini, ni mkiristo
ITAKUWA NDOA YA NNE
Wastara ambaye alizaliwa mwaka 1983, alipokuwa secondary kidato cha pili aliacha shule huko Morogoro, akiwa na miaka 16 aliolewa na mwanaume kutoka Zanzibar ambaye alimzidi sana umri ingawa ndoa haikudumu ilivunjika ndani ya muda mfupi
Baada ya kufanya kazi pamoja katika filamu kadhaa, 2008/2009 Wastara alifunga ndoa ya pili na Sajuki aliyekuwa mwigizaji wa filamu, hadi Sajuki alipoaga dunia 2013, walijaaliwa mtoto mmoja
January Mwaka 2016, Wastara aliolewa na Sadifa Juma aliyekuwa mbunge wa jimbo la Donge, Zanzibar hata hivyo ndoa yao haikudumu waliachana, hawakupata mtoto pamoja
Wastara ana watoto wengine akiwemo mmoja aliyezaa na Solo Thang mwanamuziki mkongwe wa hip-hop Tanzania ambaye kwasasa anaishi nchini Ireland kwa miaka takribani ishirini. Penzi lao lilikuwa mwanzoni mwaka miaka ya 2000s
Mbali na hayo, Wastara aliwahi pia kuwa katika mahusiano na Bond Suleiman mtangazaji na mwigizaji wa Kibongo kabla hajaolewa ghafla ndoa ya tatu hali ikiyosababisha Bond kukiri kutaka kujiu@ baada ya mrembo huyo kwenda kuolewa na mwanaume mwingine
Kwa upande wa Dudubaya alishawahi kuwa na mke kabla, pia ana watoto kutoka mahusiano yake ya awali
