Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Privaldinho ampa makavu Hans Raphael wa Crown FM

Andiko la digital Manager wa Klabu ya Young Africans Priva Abiud Shayo "Privaldinho" likimzungumzia mchambuzi wa masuala ya kandanda Hans Rafael wa Crown FM.

"Hans Hans Hans.

Mtu akipitia post zako za jana baada ya Yanga kushinda na baada ya makolo kushinda, Inafikirisha kidogo ndugu yangu. Juzi wakati makolo wanateseka dhidi ya JKT hukusema lolote baya dhidi yao. Hukuongelea chochote kuhusu Mpanzu kuwa katika mechi 8 amefunga bao moja pekee ikiwa ni mechi tatu kwenye ligi hajafanya kitu.

Hukusema ubutu wa Mukwala. Ulichagua angle ya kuwapambana makolo.

Hukujadili clear chances walizokosa makolo.

Kipind cha kwanza JKT walifanikiwa kuwadhibiti
Makolo. Makolo walipata shot on target moja tu na shot off target 1. Ulikaa kimya

Badala yake ulisifia kiwango cha baadhi ya nyota wake. Sio dhambi kusifia ila unasifiaje?

Baada ya mapambio yako, kilichofuata sio tena uchambuzi ispokuwa ukawa mhamasishaji wa makolo. Nanukuu maneno yako

“keep fighting, keep knocking, keep believing.....hiyo ndio maana halisi ya timu kubwa. Haijalishi umetanguliwa ila ni kupambana hadi dakika ya mwisho, hakika leo Simba wamecheza kibingwa, wameonyesha Mamba mentality”

Brother, JKT uliwapa hii hamasa pia? Imekuwaje? Mchambuzi unawezaje kutoa kauli za namna hii? Huoni kama unawakosea heshima JKT? Kwamba makolo walikuwa bora kwa JKT kwa tofauti ya goli 1?

Huo umwamba wa Makolo ni upi? How? Difference ya goli moja mdogo wangu? Hivi unajua katika mechi ambayo makolo walikuwa na wastani mdogo wa pasi ni dhidi ya JKT? Hivi unajua katika mechi ambazo Kolo amefunga magoli machache ni dhidi ya JkT? Hivi unajua mechi pekee ya ligi ambayo kolo ameruhusu bao ni dhidi ya JKT?

Takwimu zinaonesha wastani wao wa pasi dhidi ya JkT ni 68 watsani mdogo zaidi msimu huu.? Hizi sifa umetoa kwenye papatu papatu hii hii?

Hivi unajua baada ya mechi 6 JKt juzi ndio amefanikiwa kupata bao dhidi ya Kolo? Kwanini unatumia nguvu kubwa kuforce agenda ya kwamba makolo wanacheza vizuri kuliko Yanga? Unawaogopa? Una balance?. Sijamaliza..! Narudi".



Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa