Ruka hadi kwenye maudhui makuu

WANAYANGA WANATAKA GUSA ACHIA TWENDE KWAO, FOLZ BADILIKA

Na Prince Hoza Matua

WANAYANGA wanataka timu yao icheze mpira wa kupigiana pasi fupi fupi kwa staili ya kwenda mbele, hawataki mpira wa taratibu na kupigiana pasi za kurudi nyuma, wameshazoeshwa na makocha wao waliopita.

Tunajua kabisa kwamba Wanayanga kupata ushindi kwao sio habari ngeni, wamezoeshwa na makocha waliopita, Yanga kushinda makombe ni jadi yao wala sio kitu kigeni, vitu ambavyo kwao ni vigeni ni pale timu yao inafungwa au kutoka sare.

Kwa kifupi mashabiki wa Yanga sio watu wa mpira, hawajui kanuni za mpira, kwamba kuna matokeo aina tatu tu, kufungwa, kushinda na kutoka sare, lakini mashabiki wa Yanga wanajua tokeo moja tu la kushinda.

Ikitokea timu yao imetoka sare, kocha ananyooshewa kidole, kama sare ya kwanza wanamvumilia kama ya pili wanampa kalipio kali na kama ya tatu wanamfungashia virago, kwa kifupi hawataki matokeo ya aina mbili yatokee.

Lakini kwa sasa mashabiki wa Yanga wamebadilika kidogo, kushinda wamegeuza kama asilia yao, ila wanataka timu yao icheze kwa ku- press kwa staili ya kwenda mbele, Nasreddine Nabi alikuja na staili ya pasi fupi fupi kwa kurudi nyuma.

Enzi zake Nabi mchezaji Salum Abunakar "Sureboy" alipata nafasi kwenye kikosi chake, Sureboy aliyesajiliwa kutoka Azam FC aling' ara sana kwenye kikosi hicho, nakumbuka Sureboy alimsaidia sana Feisal Salum Feitoto.

Sureboy alichangia kumshawishi Feitoto kuipenda mchezo wa soka na hata walipokutana Yanga, kiungo huyo ambaye sasa anakipiga Azam FC alimshukuru sana na kueleza historia yake.

Nabi akiwa Yanga aliisaidia kutinga fainali kombe la Shirikisho Afrika na pia kutwaa makombe yote matatu, kwa maana Ligi Kuu bara, kombe la FA na Ngao ya Jamii, kwa kifupi historia ya Yanga kutawala mpira wa Tanzania ulianzia kwa Nabi.

Lakini baadaye Nabi aliondoka na kujiunga na FAR Rabat ya Morocco, akaja Miguel Gamondi, wengi hawakuujua ubora wa kocha huyo raia wa Argentina.

Gamondi likuja na falsafa yake ya soka la pasi fupi kwa kwenda mbele, Gamondi alikuwa muumini wa kushambulia kwa spidi na hapo ndipo Yanga ilipoambukizwa ubaya hadi Simba wakaja na neno ubaya ubwela.

Gamondi aliendeleza mazuri ya Nabi, kwani kikosi cha Yanga kilitetea Mataji yake na vile vile kufika robo fainali ya Ligi ya mabingwa Afrika, Yanga ilikuwa tishio ndani na nje ya nchi, Gamondi naye aliondolewa baada ya timu yake kupoteza mechi mbili mfululizo dhidi ya Azam FC na Tabora United.

Alipoondoka Gamondi akaletwa Sead Ramovic raia wa Ujerumami, Ramovic aliendeleza mazuri ya mtangulizi wake Gamondi na timu ikazidi kusifika, gusa achia twende kwao ilisikika ndani ya Yanga huku mashabiki wake waliendelea kifurahia.

Hata hivyo Ramovic aliondoka baada ya kupata timu Algeria, lakini Yanga walimchukua Miloud Hamdi raia wa Algeria na akaja kuendeleza yale yale ya wenzake, Nabi, Gamondi na Ramovic.

Miloud naye akaondoka mitaa ya Jangwani, wakamleta Ramon Folz, maisha ya Folz ndani ya Yanga sio mazuri, mashabiki hawafurahishwi na mfumo wa uchezaji, kwani amebadilisha kila kitu na timu haichezi tena kwa ku- press na pia haijulikani wanacheza kwa staili gani.

Kelele zimezagaa kama abiria wa mwendokasi wa Kimata mpaka Mkuu wa Mkapa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila kuwatembelea, Wanayanga kikubwa wao wanataka gusa achia twende kwao, Folz badalika.
ALAMSIKI
+255766 514 040


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.