Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Simba yampa mkono wa kwaheri Ali Salim Khatoro

KLABU ya Simba imeachana na kipa wake, Ally Salim Juma Khatoro baada ya miaka nane tangu impandishe kutoka timu ya vijana.

Mlinda mlango huyo mzaliwa wa Pemba — alipandishwa kikosi cha kwanza Simba msimu wa 2017-2018 baada ya kufanya vizuri katika timu ya vijana chini ya umri wa miaka 20.

Mara kadhaa alidaka mfululizo kama kipa namba moja baada ya makipa wa kwanza kuumia na msimu mzuri zaidi kwake ni wa 2022-2023 alipoiongoza Simba kufika Robo Fainali Ligi ya Mabingwa Afrika kabla ya kutolewa kwa penalti 4-3 na Wydad Athletics ya Morocco kufuatia sare ya jumla ya 1-1 baada ya kila timu kushinda 1-0 nyumbani kwake.

Aidha, Ally Salim ni mlinda mlango ambaye Simba haijawahi kupoteza mechi dhidi ya mtani, Yanga akiwa langoni na katika mechi mbili alizodaka zote Wekundu wa Msimbazi walishinda.

Mechi ya kwanza ilikuwa ni ya Ligi Kuu Aprili 16 mwaka 2023 Simba ikishinda 2-0,  mabao ya beki Mkongo, Henock Inonga dakika ya pili na Kibu Denis dakika ya 32 Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Mechi nyingine ni Fainali ya Ngao ya Jamii Agosti 13 mwaka 2023 alipookoa penalti tatu Simba ikishinda kwa penalti 3-1 baada ya sare ya bila mabao Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

Sifa nyingine ya Ally Salim ni kwamba pamoja na kuchukuliwa kama kipa wa akiba, lakini kila huduma yake ilipohitajika alifanya kazi yake vizuri.

Ni kwa sababu hiyo pia kuna wakati alikuwa anaaminiwa na kuwa kipa namba moja wa timu ya taifa, Taifa Stars ambako pia alikuwa anafanya kazi yake vizuri.

Japokubwa taarifa haijathibitisha— lakini inaelezwa kipa huyo anajiunga na Namungo FC iliyoachana na Benni Kakolanya, kipa mwingine wa zamani wa Simba SC.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC