Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mchezaji kipenzi wa Fadlu atambulishwa Simba

KLABU ya Simba SC imemtambulisha beki wa kushoto, Anthony Richard Mligo ambaye Agosti 6 atatimiza miaka 18 kutoka Namungo FC ya Ruangwa mkoani Lindi kuwa mchezaji wake mpya kuelekea msimu ujao.

Baada ya kukamilisha usajili wake, Mligo anapanda ndege leo kwenda mjini Ismailia nchini Misri kuungana na wezake kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya.

Mligo ni mchezaji aliyeibukia klabu ya Geita Gold msimu wa 2023/2024, kabla ya kuhamia Namungo FC msimu uliopita ambako aliendelea kufanya vizuri na kuitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20 ‘Ngorongoro Heroes’.

Chipukizi huyo alikuwemo kwenye kikosi cha Tanzania kilichotwaa ubingwa wa Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati kwa vijana chini ya umri wa miaka 20, CECAFA U20 Oktoba mwaka jana nchini akiibukia mfungaji wa michuno hiyo.

Chipukizi huyo alikuwepo pia kwenye kikosi hicho cha Ngorongoro Heroes kilichoshiriki Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) U20 nchini Misri.
Anakuwa mchezaji mpya wa saba kutambulishwa rasmi Simba SC hadi sasa baada ya beki wa kati, Rushine De Reuck (29) kutoka Mamelodi Sundowns ya kwao, Afrika Kusini, kiungo Msenegal, Alassane Maodo Kanté (24) kutoka CA Bizertin ya Tunisia, winga Mohammed Omar Ali Bajaber kutoka Polisi ya kwao, Kenya na mshambuliaji Mghana, Jonathan Sowah kutoka Singida Black Stars ya nchini.

Wengine ni wazawa, kiungo Hussein Daudi Semfuko (21) kutoka Coastal Union ya Tanga na mshambuliaji Morice Michael Abraham (21) Spartak Subotica ya Serbia.

Simba inatarajiwa kuuanza msimu kwa michuano midogo ya Ngao ya Jamii maalum kuashiria upenuzi wa pazia la msimu mpya wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara, 2025/2026 inayotarajiwa kufanyika kati ya Septemba 11 hadi 14.

Simba SC itacheza na Singida Black Stars. Septemba 11 na ikishinda itakutana na mshindi kati ya Yanga na Azam FC katika Fainali.

Baada ya hapo Simba itaingia kwenye Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara ambayo itaanza Septemba 16 – wastani wa wiki mbili tu baada ya kumalizika kwa na Fainali za Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN).


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC