Ruka hadi kwenye maudhui makuu

JOB NDUGAI ATAKUMBUKWA KWA MENGI KWENYE MICHEZO

Na Prince Hoza

ALIYEKUWA Spika wa Bunge la Tanzania na Mbunge wa Kongwa, Job Yustino Ndugai amefariki Dunia August 06,2025 akiwa anaendelea kupatiwa matibabu Hospitalini baada ya kuugua ghafla.

Ndugai amekuwa Spika wa Bunge tangu November 17,  2015 hadi Januari 06, 2022 alipojiuzulu na kuendelea kuwa Mbunge wa Kongwa  nafasi ambayo ameendelea kuitetea kwa kuchukua fomu tena mwaka huu ambapo ameshinda kwenye kura za maoni.

Ndugai ambaye amezaliwa January 22,1960 alishinda kura za maoni za Ubunge wa Jimbo la Kongwa kwa kupata kura 5690.

ALIHAKIKISHA TAIFA STARS INAFUZU FAINALI ZA AFCON MWAKA 2019

Ndugai tutamkumbuka kwenye tasnia ya michezo hasa alipokuwa Spika wa Jamhuri ya Muungano ambapo alikuwa mstari wa mbele kuhakikisha soka la Tanzania linapiga hatua.

Ikumbukwe marehemu Ndugai alikuwa sambamba na wabunge wenzake kuunda Kamati ya hamasa ambayo iliisaidia timu ya taifa kufuzu fainali za Afrika, mwaka 2019 Taifa Stars ilifuzu fainali za mataifa Afrika, AFCON zilizofanyika nchini Misri.

Nakumbuka mheshimiwa Ndugai alipambana vilivyo kuona wachezaji wa Taifa Stars wanapata stahiki zao ambazo zikasaidia kufuzu fainali, wakati hup Rais wa Jamhuri ya Muungano alikuwa Dkt John Pombe Magufuli ambaye naye ni marehemu.

ALIKUWA SHABIKI KINDAKINDAKI WA SIMBA SC

Kwa ushirikiano wao viongozi wa Tanzania, kwa maana Rais wa nchi na Spika wa nchi walihalikisha Tanzania inafuzu fainali za mwaka huo (2019) baada ya miaka 38 ilipofanya hivyo mwaka 1981 wakati fainali zake zilipofanyika nchini Nigeria.

Marehemu Ndugai atakumbukwa kwa juhudi zake kwenye michezo kwani mbali ya kulisaidia taifa katika michezo, pia alikuwa shabiki kindakindaki wa klabu ya Simba SC.

Ndugai alishiriki kuanzisha tawi la Simba SC jijiji Dodoma ambalo liliwahusu waheshimiwa wabunge, tawi hilo lilizinduliwa na aliyekuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano, Dkt Samia Suluhu Hassan ambaye kwasasa ni Rais.

YEYE NA RAIS MAGUFULI WALIWAPA VIWANJA WACHEZAJI WA STARS KWA KUFUZU

Kwa kifupi marehemu Ndugai alikuwa na mchango mkubwa kwenye soka na kifo chake ni pigo, Watanzania tumempoteza mtu muhimu na MIKASI imeona umuhimu wake na kuandika kumbukizi kwa ufupi.

Baada ya Stars kufuzu fainali za mwaka 2019, Rais Magufuli aliamua kuwazawadia wachezaji wa timu hiyo ya taifa viwanja mjini Dodoma, Ndugai ambaye ni Spika, alishiriki kikamilifu kuhakikisha wachezaji wa timu hiyo wanapewa viwanja vyao.

Tanzania imepata bahati kubwa ya kuwa na viongozi wa kisiasa ambao ni wapenda michezo, kwani Ndugai alikuwa mwanamichezo kindakindaki, kifo chake kimetushitua sana sisi wadau na mwisho tunamshukuru mwenyezi Mungu.

ACKSON TULIA AMLILIA

Taarifa ya kifo hicho zilitolewa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani, Dkt. Tulia Ackson. 

“Kwa masikitiko makubwa, naomba kutoa taarifa ya kifo cha kiongozi wetu, mwanasiasa mkongwe na Spika Mstaafu wa Bunge Mheshimiwa Job Yustino Ndugai kilichotokea leo jijini Dodoma,” amesema Tulia katika taarifa hiyo na kuongeza 

“Natoa pole kwa familia ya Marehemu, ndugu, jamaa na Wananchi wa Jimbo la Kongwa, Mwenyezi Mungu awape moyo wa uvumilivu na subira katika kipindi hiki kigumu,” amesema Spika.

Aidha amesema Ofisi ya Bunge kwa kushirikiana na Kamati ya Mazishi pamoja na familia ya Marehemu inaratibu mipango ya mazishina taarifa zaidi zitaendelea kutolewa.




Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC