Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Singida Black Stars yaridhia Sowah kwenda Simba

MSHAMBULIAJI Mghana, Jonathan Sowah (26) amejiunga na Simba SC akitokea Singida Black Stars alikodumu kwa nusu msimu tangu awasili.

Taarifa ya Singida Black Stars leo imesema kwamba wameridhia kumruhusu Sowah kujiunga na Simba SC baada ya mazungumzo baina ya watu wenye mamlaka ya juu kwenye timu zote.

Hao ni Mlezi wa Singida Black Stars, Dk. Mwigulu Lameck Nchemba ambaye pia ni Waziri wa Fedha na Mipango wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Bodi ya Simba, Mohamed Gulam ‘Mo’ Dewji ambaye pia ni Rais wa heshima wa klabu hiyo.

Sowah alijiunga na Singida Black Stars Januari 17, mwaka huu 2025 akitokea Al-Nasr ya Libya ambako alidumu kwa msimu mmoja baada ya kuwasili akitokea Medeama ya kwao, Ghana Januari 27, mwaka jana 2024.

Kisoka, haswa Sowah aliibukia Danbort FC ya kwao pia, Ghana kabla ya kuhamia Medeama SC Novemba 11, mwaka juzi, 2023.
Akiwa Medeama ndipo Watanzania walianza kumuona mchezaji huyo kufuatia klabu yake hiyo kukutana na Yanga ambao ni wapinzani wakubwa wa Simba nchini katika hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Yanga ilikuwa timu ya kwanza kuonyesha nia ya kumsajili Sowah kabla hajaenda Al-Nasr, lakini mapema mwaka huu akajiunga na Singida Black Stars huku kukiwa na taarifa kwamba atacheza kwa muda kabla ya kujiunga na Wananchi.

Inaaminika rekodi yake ya utovu wa nidhamu ilichangia Yanga kuachana na mpango wa kumsajili baada ya kugombana na mashabiki wa Simba mara mbili mfululizo katika mechi ya Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge, Dar es Salaam na Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF),
Aidha, kitendo cha kutolewa kwa kadi nyekundu katika mechi muhimu ya Fainali ya Kombe la TFF, michuano inayodhaminiwa na Benki ya CRDB kilionekana kabisa kuwafanya Yanga wajifikirie mara mbili kumsajili mchezaji huyo licha ya rekodi yake nzuri ya kufunga mabao.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...