Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Ligi Kuu bara 2025/2026 kuanza kutumia vumbi Sept 16

MSIMU mpya wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara, 2025/2026 unatarajiwa Septemba 16, mwaka huu 2025 – wastani wa wiki mbili tu baada ya kumalizika kwa na Fainali za Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN).

Msimu mpya wa Ligi Kuu umelazimika kuchelewa kutokana na Tanzania mwenyeji mwenza wa CHAN pamoja na jirani zake, Kenya na Uganda zinazotarajiwa kuanza Agosti 2 hadi 30, mwaka huu.

Ni kutokana na uenyeji wa CHAN tukio la utoaji Tuzo kwa nyota waliofanya vizuri msimu uliopita wa LIgi Kuu halijafanyika hadi sasa na pia haifahamiki kama michuano ya Nguo ya Jamii ambayo hushirikisha timu nne zilizomaliza nafasi za juu itakuwepo msimu huu.

Timu 16 zinazotarajiwa kushiriki Ligi Kuu msimu ujao ni pamoja na mabingwa watetezi, Yanga SC, Simba SC, Azam FC, Singida Black Stars, Tabora United, Coastal Union, Mashujaa, Dodoma Jiji FC, JKT Tanzania, Namungo FC, KMC, Pamba Jiji, Tanzania Prisons, Fountain Gate, Mtibwa Sugar na Mbeya City.

Katika CHAN Kundi A kuna Kenya, Morocco, Angola Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Zambia, Kundi B kuna Tanznaia, Madagascar, Mauritania, Burkina Faso na Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR), wakati Kundi C linazikutanisha Uganda, Niger,
 Guinea, Algeria na Afrika Kusini wakati Kundi D kuna Senegal, Kongo-Brazaville, Sudan na Nigeria.

Mechi za Kundi zitachezwa Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam, Kundi B zitachezwa viwanja vya Nyayo na Moi Jijini Nairobi, Kenya, Kundi C Uwanja wa Mandela Jijini Kampala, Uganda na Kundi D Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC