Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Yanga mabingwa wa Muungano


Klabu ya Yanga SC imetwaa ubingwa wa Mashindano ya Kombe la Muungano 2025 baada ya kuifunga JKU ya Zanzibar bao 1-0 katika mchezo wa fainali uliochezwa Mei 1, 2025, kwenye Uwanja wa Gombani, Pemba.

Bao pekee la ushindi lilifungwa na kiungo mshambuliaji wa Yanga, Maxi Nzengeli, katika dakika ya 45 ya kipindi cha kwanza.

Kwa ushindi huo, Yanga walijinyakulia Kombe pamoja na zawadi ya shilingi milioni 50, huku JKU wakipata milioni 30 kama washindi wa pili. Zawadi hizo zilikuwa ni sehemu ya juhudi za kuhamasisha na kuendeleza michezo nchini, na zilikabidhiwa na Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Zubeir Ali Maulid.

Mashindano ya Kombe la Muungano yameendelea kuwa jukwaa muhimu la kuimarisha mshikamano na ushirikiano kati ya Tanzania Bara na Zanzibar kupitia michezo. Ushiriki wa timu kutoka pande zote mbili za Muungano umeonyesha dhamira ya pamoja ya kukuza vipaji na kuendeleza michezo kama chombo cha kuleta umoja na maendeleo ya kijamii.

Yanga SC imewahi kutwaa Kombe la Muungano mara 7 katika historia ya michuano hiyo. Mataji hayo yalipatikana katika miaka ya 1983, 1987, 1991, 1996, 1997, 2000 na leo 2025
Simba SC nayo inashika nafasi ya pili kwa kutwaa mara nyingi Kombe hilo mara 6 ambapo mara ya mwisho ilishinda mwaka jana 2024 mbele ya Azam FC.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...