Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Shime aita 30 kujiandaa na mataifa Afrika kwa wanawake


KOCHA Bakari Nyundo Shime ameita wachezaji 30 kuunda kikosi cha awali cha timu ya taifa kwa ajili ya maandalizi ya Fainali za Kombe la Mataifa Afrika kwa Wanawake (WAFCONN 2025) ambacho kitaanza na michezo ya kirafiki katika Kalenda ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA).

Hao ni pamoja na makipa; Naijat Abbas (JKT Queens), Asha Mrisho (Mashujaa Queens) na Janet Shija (Simba Queens).

Mabeki ni; Fatuma Issa (Simba Queens), Vaileth Nicholaus (Simba Queens), Lidya Maximillian (JKT Queens), Juletha Singano (Juarez, Mexico), Esther Maseke (Bunda Queens), Anastazia Katunzi (JKT Queens), Noela Luhala (ASA Tel Aviv University, Israel) na Christer Bahera (JKT Queens).

Viungo ni; Enekia Kasonga (Mazatlan FC, Mexico), Donisia Minja (JKT Queens), Asha Ramadhan (Yanga Princess), Maimuna Kaimu (ZED FC, Misri), Janeth Christopher (JKT Queens), Suzan Adam (Tutankhamun, Misri), Agnes Palangyo (Yanga Princess), Elizabeth Chenge (JKT Queens) na Aisha Mnunka (Simba Queens).

Wengine ni Stumai Abdallah (JKT Queens), Aisha Masaka (Brighton & Hove Albion, England), Clara Luvanga (Al Nassr, Saudi Arabia), Winfrida Gerald (JKT Queens), Hasnath Ubamba (FC Masar, Misri) na Diana Lucas(Trabzonsper, Uturuki) na Mary Siyame (Fountain Gate Princess), wakati washambuliaji ni Opa Clement (Juarez, Mexico) na Jamila Rajab (JKT Queens).

Kocha Bakari Nyundo ameiambia Bin Zubeiry Sports - Online kwamba watakuwa na michezo miwili ya kujipima nguvu dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Mei 30 na Juni 2 Jijini Dar es Salaam kabla ya kwenda Morocco kwenye Fainali za WAFCON zinazotarajiwa kuanza Julai 5 hadi 26.

Twiga Stars imepangwa Kundi C pamoja na mabingwa watetezi, Afrika Kusini ‘Banyana Banyana’, Ghana ‘Black Queens’na Mali ‘The Female Eagles’, wakati Kundi A kuna wenyeji, Morocco, Zambia, Senegal na DRC na Kundi B linazikutanisha Nigeria, Tunisia, Algeria na Botswana.

Hii ni mara ya pili tu Tanzania inashiriki WAFCON Afrika baada ya 2010 ilipokuwa chini ya Kocha mwingine mzalendo, Charles Boniface Mkwasa..


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...