Ruka hadi kwenye maudhui makuu

FADLU ANASAIDIWA NA MAREFA

Na Prince Hoza

KITENDO cha Wekundu wa Msimhazi, Simba SC kutinga hatua ya fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika, sifa kemkem zinaelekezwa kwa kocha mkuu wa timu hiyo Fadlu David's raia wa Afrika Kusini.

Imepita miaka 32 Simba kuingia fainali ya michuano ya CAF, ilifanya hivyo mwaka 1993 ilipofanikiwa kuingia fainali ya kombe la CAF ambalo sasa ni Shirikisho, likiunganishwa mwaka 2004 na kombe la Washindi.

Simba ilikutana na timu ya Stella Abidjan ya Ivory Coast ambapo katika mchezo wa kwanza uliofanyika Ivory Coast timu hizo mbili zilitoshana nguvu kwa kutoka sare isiyo na mabao 0-0.

Mchezo wa pili wa fainali uliofanyika uwanja wa Taifa, sasa Uhuru jijini Dar es Salaam na Simba ilifungwa mabao 2-0 mbele ya mgeni wa heshima, Rais wa awamu ya pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Alhaj Ali Hassan Mwinyi.

Imepita miaka 32, Simba imerudia historia yake na ikifanikiwa kuingia fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika ambapo imekutana na timu ya RS Berkane ya Morocco, Simba imefungwa kwa jumla ya mabao 3-1 na kombe likielekea Morocco.

Mchezo wa kwanza uliofanyika uwanja wa Manispaa ya Berkane nchini Morocco na Simba ikakubali kipigo cha mabao 2-0, lakini fainali ya pili ilifanyika uwanja wa New Amaan Stadium Zanzibar Jumapili iliyopita na timu hizo kutoka sare ya kufungana bao 1-1.

Kwa jumla Simba imefungwa mabao 3-1, kitendo cha Simba kufika fainali, sifa zote anapewa kocha Fadlu, amefanya kitu kikubwa ambacho wengine awajafanya katika miaka ya karibuni, Dragan Popadic raia wa Yugoslavia (sasa haipo) na Abdallah Kibaden ni walimu pekee kuiongoza Simba kufika fainali mwaka 1993.

Historia ya klabu hiyo iliyoandikwa, inaitaja fainali ya mwaka 1993, kwani klabu hiyo haijawahi kufika hatua hityo kubwa, nafasi nyingine kufikiwa na Klabu hiyo ni mwaka 1974 ya kufika nusu fainali ya kombe la Klabu bingwa Afrika.

Wamepita makocha mbalimbali kwenye Klabu hiyo na ambao wengine wanaheshinika sana Afrika na dunia, lakini wameishia robo fainali ya Afrika na ikafikia kwamba Simba ilifahamika kama "Mwakarobo" kwa sababu inaishia robo fainali.

Wekundu hao wa Msimhazi msimu huu wameamua wafike mbali na kufanya mabadiliko makubwa ya kusajili wachezaji wapya na kocha mpya, Simba walienda Afrika Kusini na kumchukua kocha wa zamani wa Orlando Pirates, Fadlu David's na kuwa kocha wake mkuu.

Ni kweli- Fadlu tumemuona, ni kocha nzuri kwani ameweza kukibadili kikosi cha timu hiyo na kuweza kuleta ushindani na watani wake Yanga SC , misimu kadhaa iliyopita, Yanga ilikuwa mtawala wa soka la nchi.

Mbali ya kushinda ubingwa wa bara mara tatu mfululizo, ushindani ulikuwa mdogo toka kwa watani zake Simba, bila shaka msimu huu kidogo Simba inawapa mtihani Yanga.

Lakini nikirudi kwenye ukweli wa mambo, Fadlu anasaidiwa na waamuzi, au marefa, si kwenye michuano ya ndani, kwa maana Ligi Kuu bara, kombe la CRDB na hata Ngao ya Jamii, Simba inabebwa sana hata kwenye michuano ya kimataifa.

Simba hata kufika fainali, marefa wameibeba sana, ushindi wake dhidi ya Stellanboch ya Afrika Kusini haukustaili, Simba wamesaidiwa sana na waamuzi hivyo inanipa shida kumthibitisha Fadlu kama kocha mzuri kuliko wenzake waliopita Simba.

ALAMSIKI




Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC