Ruka hadi kwenye maudhui makuu

'SHIKAMOO MILOUD HAMDI'

Na Prince Hoza

WAKATI Yanga SC ikilazimishwa sare tasa 0-0 na JKT Tanzania katika mchezo wa Ligi Kuu bara uwanja wa Meja Isamuyo uliopo Mbweni jijini Dar es Salaam niliandika makala kwenye safu hii nikimponda vibaya kocha mkuu wa Yanga Miloud Hamdi.

Nakumbuka hiyo ilikuwa mechi yake ya kwanza baada ya kupewa mikoba kutoka kwa mtangulizi wake Sead Ramovic, Hamdi alitambulishwa siku moja baada ya Ramovic kuacha kazi na kila mmoja alilalamika sana mabadiliko ya Yanga.

Ramovic raia wa Ujerumani, aliacha kazi Yanga aliyeifundisha muda mfupi akichukua nafasi ya Miguel Angel Gamondi raia wa Argentina aliyetimuliwa.

Mjerumani huyo aliyekuwa anaifundisha timu ya TS Galaxy ya Afrika Kusini, aliamua kuacha kazi Yanga baada ya kupata ajira kubwa kwenye klabu ya CS Belouizdad ya Algeria.

Ramovic alipochukua mikoba ya Gamondi ambaye msimu uliopita alifanya mambo makubwa ikiwemo kutetea ubingwa wa bara, kombe la CRDB Cup na kuiwezesha Yanga kwa mara ya kwanza kutinga robo fainali ya Ligi ya mabingwa barani Afrika.

Yanga ya msimu uliopita ilikuwa hakamatiki kwani kama si mwamuzi kukataa bao la Stephanie Aziz Ki alilolifunga dhidi ya Mamelodi Sundown's ya Afrika Kusini kwa vyovyote Yanga ingetinga nusu fainali.

Gamondi pia alisifika kwa mchezo mzuri huku Yanga ikitumia nguvu na akili kwani wachezaji wake walikuwa na kasi sana, ushindi mkubwa wa mabao matano yalikuwa ya kawaida, hata mtani wake Simba SC alikoga 5-1.

Lakini msimu huu haukuwa mzuri kwake, licha kwamba alianxs vema msimu kwa kushinda Ngao ya Jamii kwa kuifunga Simba bao 1-0, na pia akianza ligi vema kwa ushindi wa mechi nane mfululizo.

Timu ya Gamondi iliweka rekodi ya kucheza mechi 8 bila kuruhusu bao, wachambuzi walianza kumshambulia Gamondi wakidai timu yake haichezi kandanda la kuvutia kama ilivyokuwa msimu uliopita.

Na Yanga ya Gamondi ya msimu huu ilionekana wazi wazi kwamba haichezi vizuri, vipigo viwili mfululizo dhidi ya Azam FC 1-0 na baadaye 3-1 dhidi ya Tabora United.

Uongozi wa Yanga chini ya Rais wake Injinia Hersi Said uliamua kumfuta kazi Muargentina huyo aliyopata pia kuzinoa timu mbalimbali barani Afrika ikiwemo Mamelodi Sundown's na CS Belouizdad.

Alipoondoka Gamondi, akaja Ramovic ambaye hakuwa na umaarufu wowote nchini Tanzania, Ramovic alikutana na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Al Hilal 2-0 na MC Alger 2-0 kwenye michuano ya Ligi ya mabingwa barani Afrika.

Sio siri kushindwa kwa Yanga kimataifa msimu huu kumetokana na mabadiliko hayo ya ghafla, lakini kwenye Ligi Kuu bara, Ramovic alisifika na kikosi chake kikawa kinatoa dozi, Yanga ikabadilishwa jina na sasa ikawa onaitwa "Gusa achia twende kwao".

Chakushangaza Ramovic akatimka na akatangazwa kocha mpya raia wa Algeria, Miloud Hamdi, kabla ya kutua Yanga, Hamdi alikuwa anainoa Singida Black Stars.

Ikiwa chini ya Hamdi, Yanga ikaanza na sare dhidi ya JKT Tanzania, nikiwa kwenye meza nikachukua kalamu na karatasi na kuandika makala ambayo haikuwa nzuri, kwani nilimponda waziwazi Hamdi nikidai si kocha wa mafanikio kwa Yanga.

Leo nadiriki kumwamkia "Shikamoo Miloud Hamdi", najua anastahili Shikamoo yangu kwakuwa amenizidi umri, kwani yeye ana umri wa miaka 53, akizaliwa Juni, 1971, Hamdi ni bonge la kocha aisee, sijaziona sifa zake kwa Wanahabari, lakini ni bonge la kocha.

Yanga imerudi zama za Gamondi wa msimu uliopita, ingawa timu hajaanza nayo, lakini anakwenda kutetea mataji, Ligi Kuu bara na kombe la CRDB, endapo Yanga watampa nafasi tena aiongoze timu hiyo ninaamini michuano ya kimataifa itafika mbali sana.

ALAMSIKI




Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...