Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Lusajo Mwaikenda na rekodi ya beki wa mabao mengi Ligi Kuu bara

BEKI wa Azam FC, Lusajo Mwaikenda amevunja rekodi ya msimu uliopita ya mabeki waliofunga mabao mengi zaidi katika Ligi Kuu, baada ya nyota huyo kufunga moja na kufikisha matano katika ushindi wa kikosi hicho wa 4-2, dhidi ya Kagera Sugar.

Lusajo alifunga bao hilo dakika ya 42, akiunganisha kwa kichwa kona iliyopigwa na Abdul Suleiman ‘Sopu’ na kuisawazishia Azam baada ya Hijjah Shamte kuitanguliza Kagera dakika 26, kisha Idd Seleman ‘Nado’ kupachika la pili dakika ya 58.

Kagera ilijibu mapigo na kusawazisha dakika ya 60 kupitia kwa Kassim Fekha, huku Nassoro Kapama akijifunga dakika ya 82 katika harakati za kuokoa mpira wa Lusajo na kuipa Azam bao la tatu, kabla ya Mcolombia Jhonier Blanco kufunga bao moja kali la nne katika dakika ya 87 ya mchezo.

Kitendo cha Lusajo kufunga bao moja kimemfanya kufikisha mabao matano ya Ligi Kuu msimu huu na kuivunja rekodi ya msimu uliopita, ambapo beki aliyekuwa na mabao mengi zaidi alikuwa ni Derrick Mukombozi wa Namungo FC aliyefunga manne.

Mbali na Mukombozi, mwingine aliyefunga mabao mengi zaidi msimu uliopita ni Nicholas Gyan anayemudu kucheza namba mbili na wakati mwingine akicheza kama winga wa kulia akiichezea Singida Fountain Gate aliyemaliza msimu pia na mabao manne.

Msimu huu mbali na Lusajo, mabeki wengine wenye mabao mengi ni Ibrahim Hamad ‘Bacca’ wa Yanga mwenye manne, Shomari Kapombe (Simba), Erasto Nyoni (Namungo FC), Pascal Msindo (Azam FC) na Hernest Malonga wa Singida Black Stars ambao kila mmoja amefunga mabao matatu.

Wengine wanaofuatia ni wenye mabao mawili ambao ni Wilson Nangu wa kikosi cha JKT Tanzania, Che Malone Fondoh (Simba), Yoro Diaby (Azam FC), Heritier Lulihoshi (Dodoma Jiji) na Mkongomani Andy Bikoko anayeichezea timu ya Tabora United.

Akizungumzia kiwango chake msimu huu, Lusajo alisema licha ya ubora anaouonyesha wa kufunga ila ni hatari zaidi wakati akiwa anashambulia, kwa sababu ni muda ambao wapinzani huweza kutumia gepu lililopo na kuweza kuwaadhibu wasipojipanga.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC