Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Alikiba atoboa siri ya kutofanya kazi na Lady Jaydee

Kwenye kipindi cha Crown FM - Air 20, Alikiba amefunguka kuhusu sababu ya kutowahi kufanya tena kolabo na Lady Jay Dee.

Ingawa haijawahi kufahamika wazi chanzo, Alikiba anasema tayari walishakutana hata baada ya Lady Jay Dee kusema hafikirii kolabo kati yao tena, lakini hajui ni nini hasa kilichompelekea dada huyo kutoa kauli ya kutoshirikiana naye tena.

Akizungumzia moja ya nyimbo zake kubwa zaidi, Seduce Me, Alikiba alisema wazo la wimbo huo lilitokana na mahusiano yake ya zamani na mpenzi wake ambaye kwa sasa ni mheshimiwa. Alikiba alisema mpenzi huyo alipenda sana kutumia Kiingereza na wakati fulani wakiwa pamoja kwa producer Man Water, alianza kuzungumza kwa lafudhi ya Kiingereza na kutamka maneno kama "Seduce Me"—ambapo Alikiba alianza kuimba hapo hapo. "Kila kitu huwa nachukulia kama fursa kwenye muziki wangu," alisema.

Alikiba alisimulia kuhusu mpenzi wake mwingine aliyemfundisha kifaransa. “Alinipigia nikiwa studio, nikamwambia anicheki baadaye maana nina rekodi. Nikamwomba maneno ya Kifaransa, akanitumia maandishi na voice note. Hivyo ndivyo wimbo wa Aje ilivyozaliwa.” Wimbo huo ulimpa tuzo ya MTVEMA na video yake ndio ilikuwa ya gharama zaidi kuwahi kufanya, ikigharimu dola 36,000.

Kuhusu biashara, Alikiba alieleza changamoto alizokutana nazo kwenye bidhaa za Mofaya. Alisema mkataba haukuwa sawa hasa upande wa kuingiza bidhaa kutoka Afrika Kusini na pia kutopatiwa kanuni ya bidhaa. “Nilizuia kwa sababu mkataba haukuwa unaenda sawa. Mungu akijalia mzigo utakuja.”

Kuhusu maisha binafsi, Alikiba alikanusha kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Queen Darlin. Alisema walikuwa tu marafiki wa karibu, na dada huyo alikuwa sehemu ya watu waliomuunga mkono sana mwanzo. “Tulipendana kama dada na kaka. Sasa hivi hatuna ukaribu kama zamani.”

Kuhusu Killy na Cheed, Alikiba alifananisha Kings Music na chuo. Alisema msanii anapoondoka ni kama amehitimu, hivyo si sahihi kurudi tena. “Wameshajitambulisha kama wasanii wanaojitegemea. Wasivunjike moyo.”

Alikiba alifafanua tukio la Abdu Kiba kukutana na Diamond Platnumz. Alisisitiza hakuwa na kinyongo, 'halikuwa kosa'.
(SNS)


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...