Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Taifa Stars ilijiandaa kufungwa...

Na Prince Hoza

MABAO ya Simba wa Atlasi yaliyoizamisha Taifa Stars yamefumgwa na nyota wa La Liga, beki wa Real Sociedad, Nayef Aguerd dakika ya 51' na kiungo wa Real Madrid, Brahim Díaz kwa Penalti dakika ya 58 Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Oujda. 

Hicho ni kipigo ilichokipata Taifa Stars dhidi ya Morocco, kipigo ambacho kimewasononesha Watanzania wengi, matumaini ya Tanzania kutinga fainali za kombe la dunia yanawekwa shakani na kipigo hicho.

Morocco si daraja letu kiasi kwamba kufungwa ni kama dhambi, hapana Morocco ni timu ya kiwango cha juu sana ambapo ni mapema sana kuifikia na kuiweka chini.

Malalamiko kufungwa na Morocco yanakuja kwamba hakukuwa na maandalizi hata kidogo kuelekea mchezo nao, Iko tofauti na mechi nyingine Taifa Stars inajiandaa vya kutosha, lakini mechi dhidi ya Morocco hakuna maandalizi kabisa.

Nashangaa kuona mchezo mkubwa wa kufuzu fainali za kombe la dunia dhidi ya Morocco, Taifa Stars inasafiri pasipo hamasa yoyote, nilichokiona kwa Taifa Stars ni sifa nyingi zikielekezwa kwa mtawala Wallace Karia


Shirikisho la soka nchini TFF kila kukicha lilikuwa lilipeleka sifa Kwa Karia kutokana na mafanikio aliyopata, hakukuwa na hamasa ya kuelekea kwenye mchezo huo, kipigo cha mabao 2-0 dhidi ya Morocco nimeona kama tulistahili.

Maendeleo ya timu yetu ya taifa, Taifa Stars ni duni sana ingawa hilo alionekana kutokana na mazuri yanaonekana kwenye vilabu vyetu, Simba na Yanga zimekuwa bora na kufanya kwake vizuri Tanzania inazidi kumwagiwa sifa kemkem.

Inasikitisha sana timu yetu ya taifa ikishindwa kufuzu fainali za kombe la dunia ingawa malengo yetu ni kufuzu, mbali na kufuzu fainali za kombe la dunia, timu ya taifa, Taifa Stars haifiki mbali kwenye fainali za kombe la mataifa Afrika, AFCON.

Timu hiyo imefuzu mara tatu lakini zote ikiishia hatua ya mtoano, kwa ukubwa tulinao kama nchi, tulistahili kufika robo fainali au nusu fainali, lakini tunaweza kufika fainali ama kuchukua ubingwa kabisa.

Kitendo cha Stars kuishia hatua ya makundi haifurahishi hata kidogo, vile vile Shirikisho letu kwa maana TFF alisikii uchungu na timu yake, kitendo cha kukataa kunolewa na makocha wa kigeni ni dhahiri kwamba hawataki mafanikio.

Bado Watanzania kunolewa na makocha wazawa kwa maana kwamba nchi yetu haijajitosheleza kwa kuwa na wachezaji lukuki wenye vipaji vya kutosha, bado wachezaji wa Kitanzania wanahitaji kunolewa na makocha wa kigeni.

Huwa nashangaa sana ninapomsikia Wallace Karia kuwakataa makocha wa kigeni wakati Simba na Yanga zenyewe zinapata mafanikio kwa sababu ya kunolewa na makocha wa kigeni, mbali na makocha wa kigeni, Simba na Yanga zinanufaika na wachezaji wa kigeni.

Kufungwa na Morocco ni kama tumependa wenyewe, hakukuwa na mkakati wowote kuona nchi inafuzu fainali za kombe la dunia wala kuona tunaibuka na ushindi, nyakati kadhaa zilizopita Taifa Stars iliweza kupambana na vigogo kama Morocco.

Tuliwahi kuifunga Morocco, ingawa Morocco ya leo si Ile ya wakati ule, lakini Stars ya leo imeachwa mbali sana na Stars zilizopita, TFF naona wameelekeza nguvu zake kwenye soka la vilabu na si timu ya taifa, Taifa Stars.

ALAMSIKI












Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...