Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Yanga wamepata tiba fasta


BAADA tu ya kutolewa katika Ligi ya Mabingwa Afrika, vigogo wa Yanga waliitana haraka na kufanya tathmini ya kile ambacho kimewakwamisha na kupitia kikao hicho yapo waliyoyabaini na kuna maamuzi walichukua, ikiwamo kuigusa kamati ya mashindano ya klabu hiyo.

Kwanza kwa pamoja walikubaliana kwamba timu yao ilistahili kupata ushindi dhidi ya MC Alger ya Algeria katika mechi ya mwisho ya makundi katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, wikiendi iliyopita ambayo iliwakwamisha kumaliza nafasi ya pili kwa Kundi A na kuvuka kwenda robo fainali.

Pili waligundua utaratibu wa wachezaji kufanya mazoezi wakitokea nyumbani na kisha kukutana siku chache kabla ya mechi unawapa uhuru uliopitiliza ambao unaleta athari hasi kwa timu.

Kutokana na hilo, klabu hiyo imepanga kufanya mambo mawili ambayo inaamini yatakuwa suluhisho kwa siku za usoni.

Jambo la kwanza ambalo imeamua kulifanya ni kufanya maboresho ya kamati ya mashindano na kuna baadhi ya watu itawapunguza na wengine kuongezwa ili kuipa nguvu zaidi.

"Ni maboresho ya kawaida ambayo yamekuwa yakifanyika mara kadhaa pindi msimu unapomalizika au pale na uongozi unaona kuna sehemu inayumba hivyo wala sio jambo la ajabu au la kushangaza kwa vile lengo ni timu ifanye vizuri," kilisema chanzo cha uhakika kutoka ndani ya Yanga.

Timu hiyo pia imeamua kurudisha utaratibu wa kambi kwa wachezaji wake ambayo itaanza rasmi leo huko Avic Town Kigamboni.

"Wachezaji wataingia kambini kesho (leo) na itakuwa endelevu tofauti na zamani na walikuwa wakitokea nyumbani na kisha kukutana siku chache kabla ya mechi," kilisema chanzo hicho.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC