Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Uraia pacha umeshindikana, kubadili uraia inawezekana

Na Prince Hoza

VYOMBO vya Habari hapa nchini vilikuwa vinapiga kelele kila kukicha suala la kutaka nchi iruhusu uraia pacha ili iwe rahisi kwa nchi yetu kufaidika na wanamichezo wetu wanaoishi ughaibuni kuzisaidia timu zetu za taifa.

Vilio vilikuwa vikubwa kiasi kwamba kuliomba bunge letu tukufu la Jamhuri ya muungano wa Tanzania ili kuweza kubadili vifungu vya Sheria kwenye katiba yetu iliyopo.

Lakini licha ya kuomba sana, bunge letu tukufu likashindwa kuridhia maombi hayo huku baadhi ya wabunge wakakataa maombi hayo wakidai sababu za kiusalama.

Watanzania waliona nchi kama inachelewa katika upande wa michezo, kwani kila msimu timu zetu za taifa zinatolewa mapema katika michuano mbalimbali inayoshiriki.

Timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars ni miongoni mwa timu zilizowaliza wengi baada ya kushindwa kwake kufuzu katika michuano iliyokuwa inashiriki, kwa mfano Stars ilishindwa kufuzu michuano ya mataifa Afrika, AFCON na kombe la Dunia.

Kushindwa kwake kufuzu, kuliwafanya wadau wa soka kulijia juu bunge letu kwakuwa baadhi ya wabunge ni wapenzi wakubwa wa soka, lakini malalamiko yao hayakusaidia kitu kwani walikataa.

Kwa maombi yetu na mwenyezi Mungu akasikia kilio chetu, timu zetu za taifa zimekuwa zikifuzu michuano mbalimbali inayoshiriki, Taifa Stars imefuzu mara tatu mfululizo fainali za AFCON.

Stars ilifuzu mwaka 2019 (Misti), 2023 (Ivory Coast) na mwaka huu ambazo zitafanyika nchini Morocco, licha ya kufuzu huko wachezaji ambao waliotusaidia kufuzu ni wazawa na wengine waliokubali kuchukua uraia wa nchi moja (Tanzania).

Kwenye katiba ya Tanzania, inakataza uraia wa nchi mbili, ambapo baadhi ya wachezaji wenyewe asili ya Tanzania walioko ughaibuni, wamechukua uraia wa nchi wanazoishi.

Lakini sio dhambi kwa mtu mmoja kuwa na uraia wa nchi zaidi ya moja, lakini kwa Mtanzania hilo haliwezekani, lengo la kutaka kuwe na uraia pacha ni kuisaidia timu yetu ya taifa, Taifa Stars ifanye vizuri na ikiwezekana kutwaa ubingwa wa Afrika.

Wenzetu mataifa mengine hasa yale yaliyopiga hatua yamekuwa yakifanya vizuri katika michuano ya Afrika na Dunia kwa ujumla, lakini Tanzania imekuwa ikiishia kufuzu.

Wanasema wachezaji wetu hawana quality ya kupambana kimataifa ikizidiwa na mataifa makubwa barani Afrika ambayo yana wachezaji wenye uraia pacha.

Naweza kusema baadhi ya Watanzania wamechoka na zuio hilo na wameamua kutumia njia nyingine ya kuwafanya wachezaji wa kigeni kutoka mataifa ya magharibi mwa Afrika kuchukua uraia wa hapa (Tanzania) ili kusudi iwe rahisi kuichezea timu ya taifa kama watahitajika.

Bahati mbaya ndani ya nchi hii kuna watu wenye kasumba na kila kitu kwao nongwa na kupinga chochote hata kama ni kizuri, wachezaji wa kigeni wamejitahidi sana kiasi kwamba hata Ligi yetu imeongezeka ubora wa viwango.

Hivi karibuni wachezaji watatu wa kigeni wa timu ya Singida Black Stars walipatiwa uraia na Idara ya Uhamiaji Tanzania, lakini kelele zikawa nyingi wakipinga wachezaji hao kupewa uraia, wakati uraia pacha ilishakataliwa na wakaona watumie njia hiyo.

Njia hiyo waliyoitumia ya kuwabadili uraia wachezaji wa Singida Black Stars ni nzuri na ilipaswa kupigwa ili Tanzania tuwe na quality ya wachezaji, kupinga sio rafiki kwa maendeleo ya timu zetu za taifa.

ALAMSIKI 



Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC