Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mwaka 2024 ulikuwa mzuri kwenye soka

Na Prince Hoza

BOXING Day inamalizika hii leo  baada ya jana kusherehekea X mass, nadhani mwaka 2024 unaelekea kwisha na siku kama ya leo yaani wiki ijayo itakuwa mwaka mpya.

Jumatano ijayo ni sikukuu ya mwaka mpya wa 2025, yapo mambo mazuri ambayo tumeyaona mwaka huu na pia yapo mabaya tumeyaona, lakini mazuri ni mengi tena yakufurahisha.

Kwenye mchezo wa soka ndio sehemu inayotazamwa na wengi ingawa pia kwenye mchezo wa masumbwi pia mazuri yamefanyika, bondia Hassan Mwakinyo naye ameingia kwenye rekodi ya waliofanya vizuri msimu huu.

Mwakinyo alitetea mkanda wake wa WBO kwa upande wa Afrika, hayo ni mafanikio ya nchi kama nchi, lakini mwaka huu umekuwa mzuri kwa Tanzania kwenye upande wa soka na hasa timu zetu kufuzu kwenye michuano ya Afrika.

YANGA KUFIKA ROBO FAINALI AFRIKA

Mwaka 2024 klabu ya Yanga SC kwa mara yake ya kwanza ilifanikiwa kutinga robo fainali ya michuano ya vilabu ya Ligi ya mabingwa Afrika, Yanga iliwagharimu miaka 25 kufika hatua hiyo baada ya kuvuka hatua ya makundi.

Mabingwa hao wa bara waliweza kuvuka makundi na kuingia robo fainali ambapo walikutana na timu ya Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini, hata hivyo Yanga iliondoshwa kwa changamoto ya mikwaju ya penalti.

Malalamiko mengi baada ya mchezo huo baada ya Yanga kunyimwa goli la wazi lililofungwa na Stephanie Aziz Ki, lakini pia mwaka huu Yanga kwa mara nyingine ilifaulu tena kwa kutinga hatua ya makundi kwenye michuano hiyo ya Ligi ya mabingwa.

Kwa bahati mbaya mwaka 2024 unamalizika Yanga ikiwa mkiani kwenye kundi H inaloshiriki ikiwa na timu za TP Mazembe ya DR Congo, MC Alger ya Algeria na Al Hilal Omduman ya Sudan.

Kwenye kundi lake Yanga imefikisha pointi moja, lakini ina faida ya kucheza uwanja wa nyumbani mechi mbili zilizosalia huku moja ikitoka nje ya nchi, mimi sio mtabiri siwezi kujua la mwakani ila wamejitahidi hapo walipofikia.

SIMBA KUFIKA ROBO FAINALI AFRIKA

Mwaka 2024 pia ulikuwa mzuri kwa Wekundu wa Msimbazi, Simba SC ambapo ilifika hatua ya robo fainali ya Ligi ya mabingwa Afrika, Simba ni kama wamekuwa na mwendelezo mzuri kwani hii imekuwa mazoea kwao kufika robo fainali.

Wekundu hao walikutana na Al Ahly ya Misri na wakatupwa nje, limekuwa gonjwa kwa Simba kuishia robo fainali lakini wamejitahidi na wanatakiwa kupewa kongole, mpira wa Tanzania umepanda maradufu, Simba inatajwa kuhusika.

Simba pia imefanya vizuri zaidi mwaka huu kwa kufika hatua ya makundi ya kombe la Shirikisho Afrika, kwa bahati mbaya mwaka huu unaisha Simba ikiwa nafasi tatu ikifikisha pointi 6.

TIMU ZA TAIFA ZAFUZU AFCON

Mwaka 2024 ulikuwa mzuri kwa timu zetu za taifa za mpira wa miguu kwa upande wa wanaume, Taifa Stars ilifanikiwa kufuzu fainali za mataifa Afrika, AFCON zitakazowania a nchini Morocco.

Lakini pia timu ya taifa za vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys nayo ilifanikiwa kufuzu fainali za mataifa Afrika kwa U17 ambazo zitafanyika huko huko Morocco.

Kwa kifupi mwaka 2024 ulikuwa mzuri kwa timu zetu za taifa na vilabu vya Simba na Yanga, safu ya MIKASI inauaga mwaka 2024 kwa kuupa sifa na Mungu akipenda mwaka 2025 uwe mzuri kwa timu zetu zote zikiwemo za michezo mingine.

ALAMSIKI











Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC