Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Siasa zimemuondoa Gamondi, Yanga

Na Prince Hoza

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania bara, Yanga SC hivi karibuni walifanya maamuzi makubwa na ya kushitua nchi, baada ya kumfuta kazi kocha wake mkuu Miguel Angel Gamondi raia wa Argentina na msaidizi wake Moussa Ndaw raia wa Senegal.

Yanga waliamua kumfuta kazi Gamondi na msaidizi wake baada ya mwenendo mbaya walioanza nao msimu huu, kipigo cha bao 1-0 dhidi ya Azam FC na cha mabao 3-1 dhidi ya Tabora United kilitosha kabisa kuwafuta kazi wakuu hao wa benchi la ufundi.

Kipigo hicho mfululizo ni cha kwanza kwao tangu walipoanza jukumu la kuiongoza timu hiyo iliyofanikiwa kutwaa Ngao ya Jamii baada ya kuifunga Azam FC mabao 4-1 kwenye mchezo wa fainali uliofanyika uwanja wa New Amaan Stadium Zanzibar.

Tangu kuanza kwa msimu huu, Yanga imewachukua mechi ya tisa na ya kumi kupoteza, timu hiyo ilicheza mechi nane mfululizo ikipata ushindi na iliweka rekodi ya kipekee ya kutoruhusu bao hata moja kupenya kwenye nyavu zake.

Lakini mwenendo wa kikosi hicho msimu huu haukuvutia sana tofauti na msimu uliopita ambapo timu ilikuwa inacheza vizuri na ikipata ushindi mkubwa, Yanga ya msimu uliopita ilikuwa inamfunga mpinzani mabao 5 au 4.

Ikumbukwe msimu uliopita hata mtani wake Simba walifungwa mabao 5-1 na kumtimua kocha wao, ukiondoa Simba kufungwa 5, baadhi ya timu nyingine nazo zilikutana na kipigo hicho cha goli 5.

Kwa kifupi Yanga ya msimu uliopita ilikuwa moto wa kuotea mbali, mafanikio ambayo iliyapata msimu uliopita ni kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu bara, kombe la CRDB Cup na kufika robo fainali ya Ligi ya mabingwa Afrika.

Licha ya mwenendo wake wa kusuasua, Yanga ilikuwa kileleni huku ikimuacha nyuma mtani wake Simba kwa tofauti ya pointi 5, ratiba ngumu waliyokuwa nayo ya kucheza mechi 3 na timu za Coastal Union ya Tanga mechi ikipigwa uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha na dhidi ya Singida Black Stars mechi ikipigwa New Amaan Stadium Zanzibar.

Pia Yanga itarejea jijini Dar es Salaam kucheza dhidi ya Azam FC katika uwanja wa Azam Complex Chamazi, sio siri mechi hizo zote zilichezwa kwa ukaribu na Gamondi alikuwa akilalamikia ugumu wa ratiba.

Yanga iliweza kusafiri hadi Arusha na kupata ushindi mgumu wa bao 1-0 na lakimi pia ikasafiri hadi Zanzibar na kushinda 1-0, wakarejea Dar es Salaam na kufungwa 1-0 na hapo lawama zikaanza, mechi ambayo ilihitimisha safari yake nchini ni dhidi ya Tabora United ambapo Yanga ilifungwa mabao 3-1.

Binafsi mimi sijaona ubaya ambao Gamondi alistahili kufutwa kazi, kama kufungwa kwenye soka ni kawaida, na pia sio rahisi kumuondoa kwenye mwenye rekodi kubwa kama aliyonayo Gamondi.

Gamondi ni kocha mkubwa pengine hata wote waliowahi kupita Yanga, lakini ameharibiwa heshima yake yote, rekodi ya Yanga kwa Gamondi ni kuifikisha robo fainali ya Ligi ya mabingwa Afrika msimu 2023/2024, lakini pia kumfunga mtani wake Simba mara 4 mfululizo.

Hajatokea kwenye wa namna hiyo tangu kuundwa klabu hiyo mwaka 1935, Gamondi ameondolewa kisiasa tena za mpira, sitaki kuziweka wazi kwani zinaweza kuleta tafrani ila kama ukiwa mpenzi wa soka elewa hivyo kwamba Gamondi kaondolewa Yanga kisiasa.

Siasa zipo nyingi sana, ndani ya Yanga kuna watu walikuwa hawampendi na walitaka aondoke hata leo, lakini ndani ya Simba nao hawakutaka kumuona, Gamondi alichukiwa na wote na yeye alilijua hilo, Gamondi alijua ipo siku atafukuzwa kwa uzuri wake alionao.

Endapo Gamondi angeendelea kusalia Yanga na akiendeleza makali yake, kwa vyovyote hapa tajiri wa klabu hiyo Gharib Said Mohamed maarufu GSM angekuwa shakani, kwani tayari alianza kuandamwa na mahasimu zake kibiashara na pia kisoka.

Zimepita kelele nyingi zikishutumu udhamini wake kwa zaidi ya timu moja jambo ambalo kikanuni sio kosa lakini ufanisi wa Gamondi umewafanya watu kuona kama Yanga inanunua matokeo jambo ambalo si kweli.

ALAMSIKI



Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC