Ruka hadi kwenye maudhui makuu

ANGUKO LA YANGA LINAKUJA.......

NA PRINCE HOZA

LICHA kwamba rekodi zinaendelea kuandikwa, lakini kadri siku zinavyozidi kusogea ndipo linapoonekana anguko la Yanga, hata Simba ilionekana hivi hivi na sasa imekuwa ni kawaida Simba kuwaona kwenye nafasi ya tatu au ya nne kwenye msimamo wa ligi.

Yanga inaelekea kuanguka ingawa  kwasasa ipo kileleni inaongoza Ligi Kuu Tanzania bara inayodhaminiwa na benki ya NBC, Yanga inaongoza ligi ikiwa na pointi 24 ikicheza mechi 8 na haijapoteza mchezo wowote wala haijaruhusu bao lolote.

Ukiangalia rekodi zake za msimu unaweza kudhani ni kubwa kuliko za msimu uliopita kwani rekodi ya msimu uliopita ikicheza mechi saba za mwanzo tayari ilishapoteza mchezo mmoja dhidi ya Ihefu SC ya Mbalali mkoani Mbeya.

Lakini pia rekodi za msimu uliopita kwenye ligi hiyo Yanga iliruhusu zaidi ya goli moja, tofauti na msimu huu ambapo mpaka imefikisha mechi 8 bado haijaruhusu bao lolote na ikishinda mechi zote.

Msimu uliopita Yanga SC ilikuwa moto wa kuotea mbali na ikifanikiwa kushinda mataji mawili makubwa, Yanga ilitwaa ubingwa wa Ligi Kuu bara na pia ilitwaa kombe la CRDB Cup, Yanga pia ilifika robo fainali ya Ligi ya mabingwa Afrika.

Licha ya rekodi hizo, Yanga iliwaacha hoi pale ilipokuwa ikiibuka na ushindi mkubwa katika michezo yake ya nyumbani, ilianza ligi kwa kishindo kwa kuifunga JKT Tanzania mabao 5-0, lakini ikizichapa KMC na Simba SC mabao 5-0 kila mmoja.

Vipigo vya mabao matano viliendelea kwa kila aliyekatiza mbele yake, falsafa ya uchezaji wa kikosi kinachonolewa na Miguel Angel Gamondi raia wa Argentina kiliwafurahisha mashabiki wa timu hiyo yenye maskani yake mitaa ya Twiga na Jangwani.

Miguel Gamondi kocha wa Yanga

ANGUKO LA YANGA

Kuna dalili zote Yanga SC inakwenda kuanguka, huenda si leo wala kesho ila Yanga inaenda kuanguka, samahani sana wapenzi wasomaji wa makala yangu ya MIKASI mnielewe kuwa Yanga inaenda kuanguka.

Hakuna hata mmoja anayepanda kwenye kilele cha mlima anabaki huko huko, kuna siku atashuka, anguko la Yanga linakuja pale timu yao itakapopoteza mchezo wao ligi, anguko lingine kwa Yanga ni pale itakaoovuliwa na ubingwa wa bara.

Yanga inaweza kuvuliwa ubingwa endapo washindani wake watakapopata dawa ya kumfunga, Yanga inaweza kufungwa wakati wowote kuanzia sasa kwani mwenendo wake si mzuri.

Kutoka kwenye ushindi wa mabao matano matano ya msimu uliopita na soka la kuvutia lenye kasi mithili ya farasi au swala iliwaacha hoi Simba na Azam ambao walisubiri nyuma yake wakiachwa kwa alama nyingi.


Hata msimu huu mwanzoni mwa Ligi Kuu bara Yanga imewaacha nyuma Simba na Azam, mshindani wake kwenye ligi hiyo ni Singida Black Stars, lakini ligi bado sana kwani mzunguko wa pili haujafika na lolote linaweza kutokea.

Anguko lingine la Yanga ni pale viwango vya wachezaji wake kushuka, kwa mfano kiwango cha top score wa msimu uliopita kwenye Ligi Kuu bara Stephanie Aziz Ki si cha kuridhisha, Aziz Ki msimu uliopita alifunga mabao 21 na kuwa mfungaji bora lakini sasa ana bao moja tu.

Hata viwango vya nyota wengine wa Yanga kama Khalid Aucho, Pacome Zouzoua, Clement Mzize, Mudathir Yahya, Kouassi Attoholoa Yao "Jeshi", Prince Dube vimeshuka ghafla, sijui tatizo ni nini! Lakini kwa mwenendo huu kuna uwezekano wa Yanga kupoteza mechi na ikajikuta ikiandamwa na vioigo.

Hilo linaweza kuwakuta kwani ushindi wao umekuwa mdogo, Yanga ikishinda bao 1-0 tena ikizifunga timu ndogo na dhaifu, hata Simba ambao msimu uliopita waliwafunga 5-0, lakini walipokutana tena Yanga ilishinda 1-0 tena goli la kujifunga wenyewe, ambapo beki wa pembeni Kelvin Kijili alijifunga kwa bahati mbaya.

Ushauri wangu kwa Yanga ili waendelee kuwa wafalme wa soka la Tanzania itabidi wafanye usajili kabambe kwani kuna baadhi ya wachezaji wanaonekana kupoteza uwezo wao, lakini kingine sifa zimewajaa na wanajiona wako safi kumbe wapinzani wao wamewasoma mbinu zao na sasa wanashindwa kuja na mbinu mpya....
ALAMSIKI


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC