Tukifungwa na Azam tutauza ice cream Buguruni- Abbas

Na Ikram Khamees

Afisa Habari wa Coastal Union ya Tanga amesema endapo timu yao itafungwa na Azam FC katika mchezo wa Ligi Kuu bara Jumapili ijayo basi wachezaji wake wataamua kufanya kazi ya kuuza ice cream kuanzia Buguruni Tazara kilipo kiwanda cha Azam mpaka Kariakoo.

Akizungumza leo katika kipindi cha Sports Arena kinachorushwa na Wasafi FM, msemaji huyo amedai uongozi wa Coastal Union umekutana na wachezaji na benchi la ufundi na kumaliza tatizo lililokuwepo.

"Kwasasa timu yetu ipo vizuri na tumeshamaliza tatizo hivyo timu itakayokatiza mbele yetu itakutana na kichapo, Azam FC tutakutana nayo Jumapili tutegemee kupata ushindi" alisema.

Coastal Union imetokea kufanya vibaya kiasi kwamba ikamfukuza kocha wake David Ouma raia wa Kenya, hata hivyo licha ya kumfukuza Ouma, iliendelea kufanya vibaya wmbapo imepoteza mechi mbili mfululizo na ikitoka sare moja


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

STAA WETU: JEREMIA JUMA MTOTO WA JUMA MGUNDA ALIYEIKACHA SIMBA NA KUENDELEA NA UASKARI