Simba, Al Ahli Tripoli ngoma suluhu
Wawakilishi wengine wa Tanzania katika michuano ya CAF, Simba SC usiku huu imeilazimisha sare tasa Al Ahli Tripoli ya Libya ya 0-0 mchezo wa raundi ya kwanza kombe la Shirikisho Afrika katika uwanja wa International Tripoli.
Kwa sare hiyo isiyo na mabao kunawapa nafasi Ahli ingawa mchezo wa marudiano Simba itakuwa nyumbani kwenye uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam mbele ya mashabiki wake.
Timu zote zilicheza vizuri huku zikishambuliana kwa zamu lakini hadi mwisho wa mchezo hakuna mbabe.