Mwamuzi wa zamani afariki dunia
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), kupitia Rais wake Wallace Karia, limetuma salamu za pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na familia ya mpira kutokana na kifo cha Mwenyekiti wa Chama cha Waamuzi wa Mpira wa Miguu (FRAT), Omary Abdulkadir.
Enzi za uhai wake, Abdulkadir alikuwa mwamuzi wa FIFA na baadae alikuwa mkufunzi wa waamuzi na mpaka anafariki alikuwa Mwenyekiti wa FRAT.