Mayele ainusuru Pyramids kulala kwa APR
Bao la kusawazisha la Fiston Kalala Mayele dakika ya 83 limeiwezesha Pyramids ya Misri kwenda sare ya kufungana bao 1-1 na APR ya Rwanda katika mchezo wa Ligi ya mabingwa Afrika.
Mchezo huo wa mkondo wa kwanza uliofanyika uwanja wa Pele mjini Kigali, umesababisha timu hizo kwenda kurudiana wiki ijayo Pyramids ikiwa na faida ya goli la ugenini.
APR walitangulia kupata bao dakika ya 50 baada ya Chibi wa Pyramids kujifunga