Feitoto kurejea Yanga msimu ujao
Afisa Habari wa Yanga, Ali Kamwe ameandika kupitia ukurasa wake rasmi wa X (zamani twitwer) “Wananchi mliom-unfollow Fei Toto, naomba mkamfollow tena... Mengine tutazungumza Jumamosi kwenye mechi pale Aman Complex (Zanzibar).”
Jumamosi, Yanga SC atakuwa kwenye Dimba la New Amaan Complex Zanzibar akikipiga na CBE SA ya Ethiopia katika mchezo wa marudiano wa Kombe la Klabu Bingwa Afrika.