Feitoto aiota Yanga
Kiungo mshambuliaji wa Azam FC amesema ipo siku atarejea kwenye klabu yake ya zamani ya Yanga SC.
"Ipo siku nitarejea katika klabu yangu ya zamani ya Yanga SC, kwani ninamahusiano mazuri na Rais Eng Hersi Said ni mshauri wangu, kila siku naongea nae Kama hamniamini nitawaonyesha hata SMS"
"Ofa zipo nyingi sana, suala hilo nimewaachia wasimamizi wangu, ikitokea wakapendezwa hata na Ofa kutoka Msimbazi nitacheza huko kwani niko tayari kucheza popote"
"Kinachoniumiza hapa Azam FC ni kukosa makombe, kwani naona kabisa naenda kukosa Alama ya kuacha katika klabu hii,"
Feisal Salum Fei Toto
>>Kiungo wa Azam FC