Azam FC yabanwa na Pamba Jiji
Timu ya Azam FC usiku wa leo imeendelea kuachia pointi baada ya kulazimishwa sare tasa 0-0 nyumbani mbele ya timu iliyopanda daraja ya Pamba Jiji FC ya Mwanza mchezo wa Ligi Kuu bara kwenye uwanja wa Azam Complex Chamazi nje kidogo ya Dar es Salaam.
Kwa mwenendo huo hali inaonekana si nzuri hasa baada ya kutolewa kwenye michuano ya Ligi ya mabingwa Afrika, na pia ikianzs vibaya kwenye ligi hiyo kwa kutoka sare tasa na JKT Tanzania.
Mpaka sasa Azam imefikisha pointi mbili huku wapinzani wao Simba wana pointi 6 wakiwa wamecheza mechi mbili kama wao,.Yanga nao wana pointi tatu wakiwa wamecheza mechi moja, mechi itakayofuata ni dhidi ya Simba.
Hata hivyo mwamuzi bora Tatu Malogo aliwanyima bao la wazi wazi Pamba Jiji