Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Waarabu wa Simba Al Ahli Tripoli hawa hapa

Na Ayoub Taarifa

MAJINA KAMILI ; Wanaitwa AL AHLI SC TRIPOLI kutoka Nchini Libya na wanafahamika pia kwa jina la utani la Bianco Verde (Timu ya Karne)

Timu hii ilianzishwa Septemba 19 1950, Klabu namba mbili yenye mafanikio zaidi katika soka la Nchi ya Libya

🏆 ×13 Libya Premier league
🏆 ×7 Libyan Cup
🏆 ×2 Libyan Super Cups

Wamepata nafasi ya kucheza Kombe la shirikisho msimu huu baada ya kumaliza nafasi ya tatu msimu uliopita nyuma ya Al Nassr na Al Hilal za Libya

MAFANIKIO YAO MAKUBWA ZAIDI AFRIKA

Al Ahli Tripoli wamecheza Robo fainali Ligi ya Mabingwa Afrika mara moja & Mwaka 2022 walicheza Nusu fainali Kombe la Shirikisho Afrika wakatolewa na Orlando Pirates ambao walimuondoa Simba SC kwa Matuta

1st Leg | Al Ahli Tripoli 0-2 Orlando Pirates
2nd Leg| Orlando Pirates 0-1 Al Ahli Tripoli

WACHEZAJI WAO GHALI ZAIDI
Staa wa Angola, Straika wa Magoli Agustinō Cristovao Pacienćia "MABULULU" (32) ndiye mchezaji Ghali zaidi katika kikosi hicho akisajiliwa katika dirisha hili kwa Bil 2 za Kitanzania

Mchezaji mwingine ghali zaidi katika Kikosi chao ni Winga Hamdoi El Houni (30) aliesajiliwa kutoka Wydad Casablanca kwa uhamisho wa bure ana thamani ya Mil 800+ za Kitanzania

KOCHA MKUU
Kocha mkuu wa Klabu hii ni Chokri Khatoi raia wa Tunisia ambae amewahi kupita Abu Salim ya Libya na Stade Tunisien ya Tunisia

TOP SCORER : Ahmed Mohammed Rajab Krawas (35) ndiye nyota aliefunga mabao mengi zaidi katika msimu uliomalizika (12)

Al Ahli Tripoli anatumia Uwanja wa Libya Tripoli International kama uwanja wao wa nyumbani wenye uwezo wa kuingiza watazamaji 45,000 waliokaa

Wanatumia jezi za kijani katika mechi zao za nyumbani na wanatumia rangi Nyeupe wakiwa Ugenini

▪️THAMANI YAO : Kwa mujibu wa Transfer Market thamani ya Kikosi cha Al Ahli Tripoli ni Bil 6 za Kitanzania

▪️Mara ya mwisho kwa Al Ahli Tripoli kucheza katika Ardhi ya TANZANIA ilikua ni mwaka 2021 wakipoteza 2-0 kwa Biashara United MARA


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...