Haji Mnoga akamilisha usajili Salford City

Beki wa kimataifa wa Tanzania, Haji Mnoga amekamilisha usajili wake kuelekea katika Klabu ya Salford City, iliyopo Jiji la Manchester Nchini Uingereza.

Mnoga amesaini mkataba wa mwaka mmoja (mpaka 2025) na Klabu hiyo akitokea katika Klabu ya Portsmouth kama mchezaji huru.

Salford City ni Klabu inayoshiriki Ligi daraja la pili Kiwango cha nne kwenye wa mfumo wa Ligi Nchini Uingereza.

Hivi sasa iko katika nafasi ya 20 kwenye msimamo wa Ligi hiyo yenye timu 24 katika michezo mitatu.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

STAA WETU: JEREMIA JUMA MTOTO WA JUMA MGUNDA ALIYEIKACHA SIMBA NA KUENDELEA NA UASKARI