Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Simba na Yanga sio timu za serikali

Na Prince Hoza

NIMEMSIKILIZA vizuri Rais mstaafu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete alipokuwa anazungumza na Wasafi FM kupitia kipindi cha Good Morning.

Mstaafu Kikwete nilimuelewa vema hasa pale alipoweka wazi kwamba vilabu vya Simba na Yanga- ni mali ya wananchi na si serikali kama ambavyo watu wanafahamu hivyo.

Hata mimi mwenyewe nilikuwa najua kwamba Simba na Yanga- ni timu za serikali kwakuwa zilihusika katika kugombana uhuru wa nchi hii, lakini Kikwete ametuweka wazi.

YANGA KUITWA TIMU YA CCM

Chama Cha Mapinduzi kwa kifupi CCM inatumia rangi ya kijani, njano na nyeusi ambayo pia klabu ya Yanga- SC inatumia rangi hizo hizo, mashabiki wa Yanga- hupendelea kuvaa nguo zenye rangi hizo tatu.

Lakini wanachama wa CCM nao huvaa nguo zenye rangi hizo hizo tatu, makao makuu ya Yanga- yapo Jangwani mtaa wa Twiga, Kariakoo jijiji Dar es Salaam pamepigwa rangi ya kijani, njano na nyeusi sawa na makao makuu ya CCM yaliyopo Dodoma na Dar es Salaam ofisi ndogo.

Mara nyingi timu ya Yanga- ikiwa inacheza endapo inapata goli mashabiki wake hupendelea kuitwa "CCM...CCM......CCM" hiyo ni ishara kubwa ya Wanayanga kuashiria timu yao imepata goli.

Hata kama inafungwa mahasimu wao Simba hupendelea kuwatania kwa kuwaita CCM, hiyo yote imenifanya niamini kwamba Yanga- ni timu ya serikali, kwa maana CCM ndio inayotawala nchi.

Historia ya Uhuru wa Tanganyika sasa Tanzania, baada ya kuungano na Zanzibar, Yanga- inatajwa kuhusika kwake na ndio maana timu hiyo ina chembe chembe za serikali, ni ngumu sana kuitenganisha Yanga- na serikali 

Lakini Rais mstaafu Kikwete ameweka wazi kwamba tiku hizo ni za wananchi na aina uhusiano wowote na serikali, Kikwete ameenda mbali hata Simba nayo ni timu ya Wananchi.

Amesema ni ngumu vilabu hivyo kuwa za serikali, kwani serikali haina mpango wa kuzisimamia timu zao na zikafanya vizuri, kwa mfano miaka ya nyuma mashirikisho ya umma yaliwahi kumiliki timu na zikacheza Lig  Kuu.

Lakini maendeleo yake hayakuwa mazuri kwani zilikuja kutelemka daraja, kwa mfano Reli ya Morogoro, Pamba FC ya Mwanza, Ushirika Moshi, RTC Kigoma, RTC Kagera na nyinginezo 

Pia timu za majeshi kama JKT Tanzania, Ruvu Shooting, Polisi Dodoma, Polisi Morogoro, Tanzania Prisons na nyinginezo, ufanisi wake si mzuri na zikizidiwa na timu za wananchi za Simba na Yanga.

Rais mstaafu Kikwete ameendelea kwa kutuweka wazi kwamba hata Shirikisho la soka nchini TFF ni mali ya wananchi na si ya serikali, kiongozi mkuu wa nchi wa kuanzia mwaka 2005 hadi 2015 amedai Baraza la Michezo la Taifa, (BMT) pekee ni mali ya serikali 

Serikali yenyewe inasimamia sheria tu, wananchi ndio wenye timu hizo hivyo jukumu la kuweka sheria ni wao, wapo baadhi ya mashabiki wa soka nchini wanajua kwamba Yanga- ni timu ya serikali na Simba pia ya serikali.

Ukweli ni kwamba hizo ni timu zetu wananchi, timu za wananchi zipo nyingi ila nimezitaja Simba na Yanga kutokana na mazoea, hata Coastal Union na African Sports zote za Tanga ni timu za wananchi, Pan African, Ashanti, Tukuyu Star na nyinginezo ni mali za wananchi 

ALAMSIKI



Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC