TAJIRI SIMBA AZUIA KIBU KWENDA YANGA
Na Shafih Matuwa
Habari njema kwa mashabiki wa Simba SC au maarufu kama Wekundu wa Msimbazi kwamba mchezaji wao kipenzi Kibu Denis "Mkandaji" sasa anaweza kubaki kwenye kikosi hicho msimu ujao.
Taarifa za ndani zinasema kwamba mmoja kati ya matajiri wa klabu hiyo ameweka mzigo wa fedha mezani na amepanga kumbakisha kikosini kwa kumpa mkataba wa miaka miwili.
Na tayari uzushi kwamba anaenda Yanga zimezimwa na presha ya mashabiki wa Simba zinaonekana kuisha, huku mashabiki wa Yanga roho zinawauma waliposikia tajiri huyo amezima jaribio la Kibu kwenda Yanga