Ruka hadi kwenye maudhui makuu

FREDDIE MICHAEL ATAWAUMBUA WATU HUMU!

Na Prince Hoza
0652-626627

KWA hakika kabisa hali inavyoelekea mwishoni mwa msimu huu, kuna watu watakuja kuumbuka, kuanzia wachambuzi mpaka mashabiki watakaatana wenyewe kwa wenyewe.

Hiyo yote inatokana na kauli zao wanazozitoa kwa mshambuliaji Freddie Michael Koblas raia wa Ivory Coast anayeichezea klabu ya Simba.

Mshambuliaji huyo aliyesajiliwa kwenye dirisha dogo la Januari mwaka huu sambamba na mshambuliaji mwenzake Jobe Omari raia wa Gambia.

Kwasasa Freddie na Jobe ni gumzo kubwa kwenye medani ya michezo hasa soka, wapo baadhi ya wadau tena wana majina makubwa wamefikia kuwabeza Freddie na Jobe huku wakiuponda uongozi wa Simba kwa kufanya usajili mbaya zaidi.

Kitendo cha Simba kuwatema washambuliaji Jean Baleke na Moses Phiri ambao walikuwa na rekodi nzuri za kufunga, kuliwaudhi wengi walioamini kwamba Jobe na Freddie wanaweza kuwazidi uwezo nyota hao.

Baleke raia wa DR Congo alijiunga na Simba akitokea TP Mazembe ya mjini Lubumbashi na Phiri raia wa Zambia aliyekuwa anaichezea timu ya Zanaco.

Simba iliamua kuwaacha washambuliaji hao kwa sababu haifanyi vizuri na ilishindwa kufikia malengo yake kwenye michuano ya kimataifa hasa Ligi ya mabingwa Afrika.

Lakini Baleke alikuwa na msimu mzuri kwenye Ligi Kuu bara ila kimataifa hakuwafurahisha Wanasimba, sawa na Phiri naye namba zake hazikuwa nzuri kimataifa ila kwenye ligi ya bara inasomeka.

Hivyo wawili hao wakaondoka na Jobe na Freddie wakatua Msimbazi, kadri siku zilivyozidi kusonga mashabiki wa Simba wakajigawa makundi mawili, wapo wanaomkataa Freddie na wapo wanaompa muda.

Baadhi ya wachambuzi nao wanamkataa Freddie wakidai Simba sio daraja lake, hata baadhi ya viongozi wa klabu hiyo nao wanamkataa Freddie tena wakiponda usajili wake na wakidharau kwamba mchezaji huyo hata Tandale anapatikana.

Hata hivyo Freddie anawajibu kwa vitendo, kwenye Ligi Kuu ameshafunga jumla ya magoli manne, moja akiifunga Yanga SC.

Freddie amekuwa na wastani mzuri wa kufunga, kwani ni mechi tatu mfululizo amefunga, Freddie ndiye mfungaji kwenye mchezo dhidi ya Ihefu (Singida Black Stars) na pia ni mfungaji dhidi ya Yanga na jana alifunga dhidi ya KVZ mchezo wa Ligi ya Muungano.

Mpaka sasa Freddie amefunga mabao tisa kwenye mashindano yote aliyocheza, wanaomkataa Freddie wajiandae kwa aibu kwani jamaa anajua kufunga na anaweza kufanya makubwa zaidi pindi atakapopewa muda

ALAMSIKI

Freddie Michael Koblas

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC